Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Je, Serikali imefikia hatua gani katika mradi wa kutoa maji kutoka Nzega Mjini, tenki la Ushirika hadi Bukene ambapo vijiji 20 na vitongoji zaidi ya 100 vitanufaika?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, yanayoleta matumaini kwa wananchi zaidi ya 80,000 katika vijiji 20 vya Jimbo la Bukene ambao sasa wanakwenda kupata majisafi na salama kutoka Ziwa Viktoria: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari baada ya Bunge hili la bajeti tuongozane kwenda Bukene ili apeleke hizi taarifa njema na kuwaandaa wananchi kupokea mradi huu muhimu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nakushukuru sana kwa kupigilia msumari ruhusa ile ya Spika aliyoiongea jana.

Mheshimiwa Naibu Spika, basi napenda tu kukuhakikishia, kwenda kwenye majimbo yenu Waheshimiwa Wabunge ni moja ya majukumu yangu. Hivyo, baada ya Bunge hili Bukene nitafika, tutafanya kazi vizuri kwa pamoja, lengo ni kuona majisafi na salama yanapatikana bombani kwa wananchi wetu. (Makofi)

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Je, Serikali imefikia hatua gani katika mradi wa kutoa maji kutoka Nzega Mjini, tenki la Ushirika hadi Bukene ambapo vijiji 20 na vitongoji zaidi ya 100 vitanufaika?

Supplementary Question 2

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa fedha za ujenzi wa mradi wa maji ya Ziwa Viktoria kutoka Ziba, Nkinga zipo: Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi huu wa kupeleka maji maeneo hayo?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mradi huu alioutaja wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea maeneo yote ambayo ameyataja, tunatarajia kuutekeleza mwaka ujao wa fedha 2021/2022.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Je, Serikali imefikia hatua gani katika mradi wa kutoa maji kutoka Nzega Mjini, tenki la Ushirika hadi Bukene ambapo vijiji 20 na vitongoji zaidi ya 100 vitanufaika?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. ISACK A. KAMWELWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwenye jibu lake la msingi la swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mjini Mpanda amezungumzia chanzo cha maji cha Bwawa la Milala. Bwawa la Milala linaweza likatoa maji kwa muda wa miezi minne tu.

Je, haoni kwamba, itakuwa ni kupoteza pesa kuwekeza katika chanzo ambacho kitatumika kwa muda wa miezi minne tu badala ya kwenda moja kwa moja kuchukua maji kwenye Ziwa Tanganyika? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru, lakini nimpongeze sana sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa namna anavyojibu maswali vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu ina rasilimali toshelevu zaidi ya bilioni 126 mita za ujazo. Sasa mkakati wa Wizara ni kutumia rasilimali toshelevu kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya majisafi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ambaye ni Waziri wangu ambaye amenifunza mpaka leo nipo hapa, hili jambo tunalizingatia katika kuhakikisha kwamba wananchi hawa tunaenda kuwaondolea tatizo hili. Ahsante sana. (Makofi)