Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Water and Irrigation Wizara ya Maji 374 2021-06-04

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-

Je, Serikali imefikia hatua gani katika mradi wa kutoa maji kutoka Nzega Mjini, tenki la Ushirika hadi Bukene ambapo vijiji 20 na vitongoji zaidi ya 100 vitanufaika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali imekamilisha kazi ya usanifu wa mradi wa kutoa maji katika tenki la Ushirika Mjini Nzega kwa ajili ya kuhudumia watu zaidi ya 79,485 katika vijiji 20 na vitongoji vyake. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha fedha shilingi bilioni mbili kimetengwa na utekelezaji wa mradi huu utaanza, ambapo utahusisha kulaza mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilometa 176, kujenga matenki matano ya kuhifadhi maji ya ujazo wa lita 100,000, lita 150,000, lita 250,000 na lita 300,000 na kujenga vituo vya kuchotea maji 83.