Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza mradi wa kuyatoa maji toka Ziwa Tanganyika na kuyapeleka katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na ninalo swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, uzoefu unaonyesha maeneo mengine duniani ikiwemo China kwa kutumia vyanzo vya kudumu imeweza kuiunganisha nchi yake kutoka kaskazini kwenda kusini kwa vyanzo vya maji. Tanzania tuna Ziwa Nyasa, Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika; ni lini Serikali itatumia vyanzo hivi muhimu kuiunganisha nchi? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Maziwa makuu ni moja ya mikakati ya Serikali kuweza kutumika na kuwa suluhisho la tatizo la maji katika nchi yetu. Hivyo, napenda kukuhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Ziwa Tanganyika katika eneo lako litatumika kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza mradi wa kuyatoa maji toka Ziwa Tanganyika na kuyapeleka katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI M. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Wakati tunasubiri mradi wa kuyatoa maji Ziwa Tanganyika kupeleka Mpanda Mjini, Serikali iliahidi kutupatia shilingi milioni 240 kwa ajili ya kukarabati vyanzo vya maji na kuhakikisha vijiji vile ambavyo vilitakiwa vipate maji, vinapatiwa maji:-

Je, Serikali inatupatia majibu yapi kupeleka hizo fedha shilingi milioni 240?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wizara tuliahidi hizi fedha ziweze kwenda kusaidia kukarabati miundombinu muhimu ili vile vijiji viweze kupata huduma.

Mheshimiwa Mbunge hizi fedha mapema tunavyoanza mwaka wa fedha 2021/2022 zote zinatumwa katika Wilaya yako, lengo ni kuona kwamba ule mradi unakarabatiwa na wananchi wanapata maji safi na salama.