Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Water and Irrigation Wizara ya Maji 373 2021-06-04

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza mradi wa kuyatoa maji toka Ziwa Tanganyika na kuyapeleka katika Manispaa ya Mpanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Mpanda ni miongoni mwa miji itakayonufaika na mradi wa miji 28 kupitia mkopo wa Dola za Kimarekani milioni 500 kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim ambapo utekelezaji wa mradi huu kwa Mji wa Mpanda utahusisha matumizi ya chanzo cha maji cha bwawa la Milala lililopo katika Manispaa ya Mpanda kwa kujenga chujio na miundombinu mingine. Mradi huu unatarajiwa kuanza mwaka huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mpango wa muda mrefu, Serikali ina mpango wa kutumia Ziwa Tanganyika ili kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Mpanda na maeneo mengine ambayo itakuwa rahisi kutumia ziwa hilo.