Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni, Mziha hadi Turiani, Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. REUBEN N. KWAGILWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Swali langu la msingi lilikuwa: Ni lini, Serikali kwa kiasi kikubwa inatoa maelezo ya kipande cha barabara cha Magole – Turiani badala ya Handeni – Mziha –Turiani. Naomba kurudia: Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kipande hiki cha Handeni – Mziha – Turiani? La kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; tunayo barabara inayofanana na hiyo ya kutoka Handeni – Kibilashi – Kiteto – Kondoa – Singida, mikoa minne inaunganisha barabara ile; Na bomba la mafuta linalotoka Hoima mpaka Tanga linapita kwenye barabara hiyo: Ni lini Serikali pia itaanza ujenzi wa barabara hiyo muhimu? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati njema sana, kwenye bajeti ya Wizara hii tarehe 27, 28 mwezi uliopita Mheshimiwa Waziri alisimama hapa kwenye Bunge Tukufu akataja kwamba tumepata kibali cha barabara 16 kati ya barabara 29 na barabara hii ya Handeni – Kibilashi – Kiteto – Kondoa – Singida imetengewa kuanza ujenzi wa kilometa 25 na wakati wote kuanzia sasa itatangazwa, ipo kwenye mchakato mbalimbali wa kisheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Wabunge wa maeneo ya Mkoa wa Tanga, Dodoma, Manyara na Singida ni kwa sababu tumepata activation kubwa, bomba la mafuta linapita hapa na mmeshuhudia Mheshimiwa Rais Museveni amekuja hapa na Mheshimiwa Mama Samia walikuwa pamoja wameweka sahihi ya ujenzi wa bomba hili la mafuta. Maana yake ni kwamba barabara hii ni lazima ijengwe ikamilike ili huduma hii iweze kufanya vizuri. Kwa hiyo, msiwe na wasiwasi ujenzi wa barabara hiyo utakamilika mapema sana. (Makofi)