Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 371 2021-06-04

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni, Mziha hadi Turiani, Morogoro?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Handeni – Mziha – Turiani yenye urefu wa kilometa 109.36, inahudumiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Handeni – Mziha – Turiani umekamilika. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 imetengwa shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kulipa sehemu ya madai ya mkandarasi wa barabara ya Magole – Turiani yenye urefu wa kilometa 45.2 na kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Turiani – Mziha – Handeni yenye urefu wa kilometa 104.0 kwa kiwango cha lami. Ahsante.