Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani mahususi wa kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana wanapomaliza vyuo vikuu? (b) Je, ni kwa nini vijana hao wasitumie vyeti vyao kama dhamana kupata mikopo ili wajishughulishe na shughuli mbalimbali za kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia hapo Mheshimiwa Naibu Waziri ameweza kuonesha programu mbalimbali na nyingi ambazo Serikali inaendelea kuzifanya kwa ajili ya kuwasaidia vijana. Sasa wanasema wakati mwingine kuona ni kuamini. Hebu anieleze sasa: Ni lini Serikali walau itaanzisha hata programu moja katika Jimbo langu ili vijana wangu nao waweze kuona haya mengi ambayo Serikali imeweza kuyazungumza? (Makofi)

Swali la pili; kwa kuwa vijana wanaopata umri wa miaka 18 kwenda juu wapo wengi; na mojawapo ya jukumu kubwa la Serikali ni kuhakikisha kwamba vijana wanapata ajira: Je, ni kwa nini sasa Serikali isiwe na ule utaratibu kama iliyokuwa nao wa JKT wa crash programe ya miaka miwili au mitatu huko huko wanajifunza ukakamavu, kilimo, ufugaji wa samaki na mafunzo mbalimbali ili baada ya hapo Serikali iwape mitaji waweze kuendelea na maisha yao? (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kwanza kumshukuru sana Mheshimiwa Mbunge Vedastus Mathayo Manyinyi kwa namna anavyojitolea katika kuhakikisha vijana katika Jimbo lake na nchi yetu wananufaika na progamu mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile napenda kumhakikishia na kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba Serikali kupitia bajeti ambayo mmetupitishia ambayo itaenda kutekelezwa kuanzia mwezi wa Saba mwaka huu tutapeleka programu ya greenhouse katika mikoa tisa iliyobakia ikiwemo Mkoa wa Mara na tutajenga greenhouse hizi katika kila Halmashauri. Kwa hiyo na Musoma Mjini ambapo anatoka kaka yangu Mheshimiwa Vedastus Mathayo Manyinyi itapata greenhouse hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile programu hizo za uanagenzi tutafanya na vyuo mbalimbali vilivyopo Mkoa wa Mara ikiwemo Chuo kile cha Lake Victoria na vyuo vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu sana na wenzetu wa JKT. Utakumbuka pia katika wasilisho la bajeti la Wizara ambayo inahusika na masuala haya ya JKT, Waheshimiwa Wabunge tulipokea ushauri wenu kwa kuona namna ambavyo JKT inaweza ikatusaidia katika kuwajenga vijana na kuwaandaa kikamilifu ili waweze kujiajiri na kuajiriwa na hata kuajiri wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. Ahsante. (Makofi)