Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo la Sumve?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru, kwa kuwa Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kuanza upembuzi yakinifu tangu mwaka wa fedha 2019/2020, 2020/2021 na leo mwaka 2021/2022 lakini upembuzi yakinifu huu hauishi na umechukua zaidi ya miaka mitatu kwa mradi huu wa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria kwenda kwenye Miji ya Malya, Sumve na Malampaka.

Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuwaambia uhalisia watu wa Sumve ili wajue ni lini wanapata maji haya ya bomba kutoka Ziwa Victoria?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria yameshafika kwenye Mji wa Ngudu na Serikali imejenga pale tenki la maji la lita milioni mbili na Naibu Waziri aliwahi kutembelea tukiwa naye; na katika mradi ule usanifu unaonesha maji yanatakiwa yafike katika Jimbo la Sumve katika Kata za Lyoma, Malya, Mwagi, Nyambiti na Wala.

Je, Serikali inasema nini kuhusu kusambaza maji haya ya bomba kwenye Kata hizo za Jimbo la Sumve?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasalali Emmanuel kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mradi wa maji wa Ziwa Victoria kufikia Kata ambazo zipo ndani ya Jimbo la Sumve, tayari Wizara inaendelea kuona uwezekano wa kukamilisha hilo na mara fedha itakapopatikana suala hili tunakwenda kulitimiza.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili tenki ambalo limekamilika usambazaji wa maji katika maeneo yale ya wakazi, suala hili tayari linafanyiwa kazi. Wizara tumeshaagiza mamlaka husika pale Mwanza na wataendelea kufanyia kazi kwa haraka sana kwa sababu tayari fedha nyingi ya Serikali imeshatumika, hivyo tunahitaji kuona kwamba wananchi wale wanakwenda kunufaika na kufaidi maji haya ambayo tunatarajia yatoke bombani.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo la Sumve?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, naomba niulize Serikali ni lini kupitia Wizara ya Maji itapeleka maji kutoka Ziwa Victoria katika Mji wa Bihalamuro kama alivyoahidi Hayati Rais Magufuli mwaka jana akiwa anaomba kura kwa ajili ya kuwatua ndoo wakina mama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver, Mbunge wa Viti Maalum, Kagera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maji kutoka Ziwa Victoria yanatarajiwa pia kunufaisha wakazi wa Jimbo la Biharamulo na hii binafsi nilishaenda kufanya ziara maeneo ya Biharamulo na mipango mikakati inakwenda ukingoni sasa ili tuweze kuona mwaka ujao wa fedha kadri ambavyo fedha itakuwa ikipatikana, Biharamulo nao wawe wanufaika namba moja.

Mheshimiwa Spika, nipende kumpongeza Mheshimiwa Oliver amekuwa mfuatiliaji mzuri na sisi hatutakuwa kikwazo, tutahakikisha wote ambao mnafuatilia kwa kina hii kazi ya usambazaji maji na kuleta maji kutoka Maziwa yetu Makuu ikiwa ni mpango mkakati wa Wizara kutumia Maziwa Makuu inakwenda kutimia. (Makofi)