Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 41 Water and Irrigation Wizara ya Maji 346 2021-06-01

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo la Sumve?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni, Mbunge wa Sumve kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, huduma ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Kwimba kwa kutegemea visima virefu ni asilimia 72 ambapo Vijiji vya Mwabaratulu, Nyashana na Sumve Mantare, Ishingisha, Mwabilanda, Nyambiti, Isunga, Kadashi na Malya vinapata huduma ya maji kutoka kwenye vituo 122 vya kuchotea maji na wateja wa majumbani ni 1,208.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali itakamilisha usanifu wa kina wa mradi wa maji kwa ajili ya kuhudumia Miji Midogo ya Malampaka, Malya na Sumve na vijiji katika maeneo hayo ambavyo huduma ya maji haitoshelezi. Usanifu huu unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Desemba, 2021 na utekelezaji wa mradi utaanza kutegemeana na upatikanaji wa fedha.