Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante na nashukuru sana kwa majibu ya Waziri, lakini sasa napenda nijue ni lini zoezi hili litaanza la ujenzi wa hiyo barabara? Naomba kupatiwa majibu. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Minza Mjika kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika jibu langu la msingi nimeainisha kwamba tayari tumeshaanza ujenzi kwenye baadhi ya maeneo na katika bajeti tutakayoanza kuitekeleza ambayo Bunge lako limepitisha, tumetenga fedha, kwa hiyo, mara tu bajeti itakapoanza kutumika barabara hiyo itaanza kujengwa, ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali ilianza ujenzi wa barabara ya lami inayotoka Sanya Juu kwenda Kamwanga ambapo ingeungana na nyingine inayotoka Rombo kuja mpaka Kamwanga na barabara hii imesimama ujenzi wake pale Kijiji cha Elerai wakati zimebaki zimebaki kilometa 42.8 tu kukamilika.

Naomba kufahamu Serikali itaendeleza lini ujenzi wa barabara hii ambayo sasa ni mwaka wa pili tangu isimame?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kiruswa, Mbunge wa Longido kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni kati ya barabara ambazo zimeainishwa kwenye bajeti yetu na kama tulivyoahidi kwenye bajeti zetu tuna uhakika bajeti itakavyoanza kutekelezwa basi itaendelea kutekelezwa kama tulivyoahidi kwenye bajeti yetu ambayo imepitishwa, ahsante.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, wananchi wa Jimbo la Mlimba ukiwauliza tatizo lao kubwa ni barabara unaweza kuacha yote lakini barabara ni kipaumbele cha kwanza.

Naomba niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo kwa niaba ya wananchi wa Mlimba; ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi rasmi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Ifakara - Ng’ambo - Mto Lumemo mpaka Lupembe Madeke yenye urefu wa kilometa 223? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ambayo ambayo ameitaja inayoanzia Mikumi, Ifakara, Mlimba, Madeke hadi Lupembe na hadi Kibena Junction ni barabara inayounganisha mikoa miwili na imetengewa fedha kwenye bajeti ambayo itaanza kutekelezwa kuanzia upande wa Njombe na kuanzia upande wa Jimbo lake kwenye sehemu mbili.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mara bajeti itakapoanza kutumika kama tulivyoahidi kwenye bajeti barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa barabara ya kutoka Bariadi - Itirima - Mwandoya mpaka Isibiti Iguguno ni kilometa 289 na iko kwenye Ilani. Je, ni lini Serikali itaanza kuijenga kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara anayoisema inatoka Mwandoya junction kwenda Mwandoya ni barabara ambayo ilikuwa bado haijafanyiwa usanifu wala upembuzi yakinifu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha huu barabara hii imepangwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili iwe sasa tayari kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nikisikia barabara inayotoka Simiyu kuja Kolandoto ni kama inanitonesha vile kidonda. Mheshimiwa Naibu Waziri ulisema tender itatangazwa; je, lini mnatangaza tender kwa barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara anayoisema ya Mbulu na hasa Mbulu Hydom yenye kilometa 50 ipo kwenye mpango wa kutangazwa kabla ya mwisho wa bajeti ya mwaka huu. Kwa hiyo, taratibu zote za manunuzi zote zinakamilisha, muda wowote barabara hii itatangazwa kabla ya kuanza bajeti ya mwakani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ambayo pia Mheshimiwa aliombea kupiga sarakati itatangazwa kabla ya mwisho wa mwaka huu, ahsante.