Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 339 2021-05-31

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-

Je, ni lini barabara kutoka Kolandoto hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge Viti Maalum, Simiyu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kolandoto hadi Meatu ni sehemu ya barabara ya Kolandoto – Lalago – Mwanhuzi – Sibiti hadi Oldeani Junction yenye urefu wa kilometa 328. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii ulishakamilika na ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha.

Katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni 5,000 zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Kolandoto – Mwanhuzi yenye urefu wa kilometa 62.5 na kipande cha Lalago – Ng’oboko – Mwanhuzi yenye urefu wa kilometa 74.

Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa Daraja la Mto Sibiti pamoja na barabara unganishi kwa kiwango cha lami zenye urefu wa kilometa 25 mpakani mwa Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu na Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida ni hatua za awali za ujenzi wa barabara hiyo ahsante.