Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza:- (a) Je, nini sababu ya barabara ya Kibiti – Lindi kuharibika mara kwa mara licha ya kufanyiwa ukarabati? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatiza hilo ili kuzuia ajali za mara kwa mara katika barabara hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; ni barabara nyingi sna Tanzania hii unakuta zimeharibika na zinasababisha ajali. Nilitaka kujua mpango mkakati maana yake Waziri amekiri kwamba ni kwa sababu ya malori yenye mizigo mizito yanapita yanasababisha uharibifu wa barabara.

Mheshimiwa Spika, mpango mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba barabara zinajengwa kwa kiwango cha lami ambayo itastahimili haya malori ambayo yanakuwa yanapita na mizigo mikubwa na kuharibu barabara na hivyo kusababisha ajali nyingi na kupoteza maisha ya watu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa sababu Serikali ina project ambayo inaendelea ya SGR na vitu vingine. Ni lini itakamilika sasa ili mizigo mingi iweze kusafirishwa kwa njia ya reli na siyo kutegemea barabara ili barabara ziweze kutumika kwa usafiri wa mabasi na magari mengine madogo madogo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati wote tunapofanya design ya barabara tunategemea na kiasi cha mizigo itakayopita na ukubwa wa barabara. Lakini kwa sababu ya mabadiliko ya uchumi kumekuwa na mabadiliko makubwa sana ya uchumi ambayo yanapelekea magari ambayo yalikuwa yamepangiwa kupita barabara hiyo hayabadiliki na hivyo lazima tubadilishe design na ndiyo maana tunafanya matengenezo na tunapofanya matengenezo kwenye barabara hizi tunahakikisha tunapofanya matengenezo ambayo sasa magari makubwa na mazito yatapita kwenye barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mkakati wa Serikali ni kufanya rehabilitation kubwa kwenye hizi barabara ambazo tunaamini zitachukua magari makubwa na yenye mizigo mizito.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba Serikali imekuwa ikisimamia na imeendelea kutoa fedha na ni mpango wa Serikali kuanzisha ujenzi wa SGR ili kunusuru barabara zetu na kuhakikisha kwamba mizigo mikubwa sasa badala ya kupita kwenye barabara ipite kwenye reli ya kisasa ambayo SGR na ndiyo maana tayari sasa barabara inaendelea kujengwa na fedha zinaendelea kutolewa ili kupunguza mizigo mikubwa itakayopita kwenye barabara zetu na kunusuru hizo barabara, ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza:- (a) Je, nini sababu ya barabara ya Kibiti – Lindi kuharibika mara kwa mara licha ya kufanyiwa ukarabati? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatiza hilo ili kuzuia ajali za mara kwa mara katika barabara hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kusini ile tunayoita ya Kilwa-Mtwara nilizungumzia hapa ni barabara mbovu kuliko barabara nyingine zote. Sambamba na hilo tunawashukuru Serikali kwa kututengea hizo pesa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo. (Makofi)

Sasa swali langu ni kwamba Serikali imesema imetoa ushauri tusafirishe hiyo mizigo kwa njia ya bandari; je, meli ya mizigo kwa ajili ya kusafirisha hiyo cement iko tayari au lini itakuwa tayari?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, azma ya Serikali ni kuboresha usafirishaji na ndiyo maana Bandari ya Mtwara imepanuliwa ili iweze tu si kusafirisha mizigo mikubwa lakini pia kufungua Mikoa ya Kusini.

Mheshimiwa Spika, kwenye bajeti na tumesema tutakuwa na ujenzi wa meli kubwa itakayokuwa inafanya pwani ya Bahari ya Hindi, lakini nilichosema kwenye jibu langu la msingi, ni kuwahamasisha wafanyabiashara wa ndani na wa nje sasa kutumia bandari yetu, kutumia meli mbalimbali za kibiashara ambapo bandari hii ya Mtwara ina uwezo wa kupokea meli kubwa na uwezo wa kushusha shehena kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge na wale ambao wanafanyabiashara; kupitia Bunge lako napenda kuwataarifu kuwa Bandari ya Mtwara sasa iko tayari kupokea mizigo mbalimbali kwa ajili ya kusafirisha hiyo mizigo na kupunguzia uzito barabara yetu ambayo sasa inaharibika mara kwa mara, ahsante. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza:- (a) Je, nini sababu ya barabara ya Kibiti – Lindi kuharibika mara kwa mara licha ya kufanyiwa ukarabati? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatiza hilo ili kuzuia ajali za mara kwa mara katika barabara hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa na mimi nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii inaharibika sana kutokana na malori hasa ya Dangote na malori ya gypsum. Lakini usafirishaji kama anavyosema ni kweli Bandari ya Mtwara imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, lakini gharama ya usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye Bandari ya Mtwara na Bandari ya Dar es Salaam ni sawa sawa na ndiyo maana wafanyabiasha wana option kusafirisha mzigo kwa barabara kuja kusafirisha kwa Bandari ya Mtwara na ndiyo maana hata mafuta watu wa mafuta wameambiwa wachukulie Mtwara, lakini bado malori ya mafuta yanatoka Tunduru, yanatoka Liwale, yanatoka Nachingwea yana option kuja Dar es Salaam badala ya kuchukulia Mtwara.

Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali sasa Serikali wataangalia namna yaku-adjust hizi bei ili iwe kivutio kwa Bandari ya Mtwara? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Kwanza majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu ni sahihi lakini niongezee tu kusema kwamba tumeshafanya mazungumzo ni kweli barabara imeharibika kwa sababu ya mzigo mzito wa Dangote lakini pia na tungependa pia hata korosho zisafirishwe kupitia Bandari ya Mtwara. Tumefanya ziara pale, tulikuwa na changamoto ya gharama ambayo Dangote alilalamika tumefanya negotiation tumekubaliana kupunguza gharama hizo.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili wenzetu wa korosho wanasema kwamba kulikuwa hamna makontena tumewapa nafasi katika Bandari ya Mtwara ili waweze kuhifadhi korosho zao na kwa sababu hiyo tunaamini kwamba hata mazungumzo yakikamilika mzigo utapita sehemu kubwa pale. Tumeboresha Bandari ya Mtwara lakini pia na uwanja wa ndege unaboreshwa, kwa kweli barabara ile kwa namna ilivyo ikiendelea kutumika vile ilivyo watu wa Kusini wataendelea kupata gharama kubwa ya mizigo yao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna shida kwamba hata uiharibifu wa barabara gharama yake ambayo inachangiwa
hatuwezi ku-replace kwa hiyo alternative njia nzuri ni kuhakikisha kwamba bandari ile inatumika vizuri na imeshaboreshwa tumetumia gharama kubwa zaidi, hayo mengine mazungumzo ya kiutawala itakamilika ili mizigo iweze kupita kwenye eneo hilo, ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza:- (a) Je, nini sababu ya barabara ya Kibiti – Lindi kuharibika mara kwa mara licha ya kufanyiwa ukarabati? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatiza hilo ili kuzuia ajali za mara kwa mara katika barabara hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, suala la barabara hii ya Kusini liko serious kuliko namna ambavyo Serikali wanafanya kulijibu hapa na niwasihi sana Serikali hayo majibu mnayoyatoa hapa si sawa; ni kuwakejeli wananchi wa Kusini. Hii barabara imeharibika sana, kuna fedha mnapeleka kwa kweli ni uhujumu wa uchumi wa watu wa Kusini. Mtakumbuka mpaka ilifikia wakati Rais Magufuli akaja akafukuza watu yaani mpaka Rais anakuja anapita anaona ubovu anafukuza watu.

Mheshimiwa Spika, kinachoendelea kwenye ukarabati ni kuongeza ubovu ndani ya ubovu yaani kwa kweli Kusini kwa sasa kumefungika.

Mheshimiwa Spika, hoja yangu ni kwamba ni lini Serikali watakuwa serious waache kutumia rasilimali za nchi hii kuharibu zaidi ile barabara badala yake waende kufanya jambo la kuonyesha wako serious na kukarabati hii barabara badala ya majibu haya mnayotoa? (Makofi)

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, nimesikiliza sana, sana hoja zilizojengwa na Wabunge na hasa katika eneo la Ujenzi wa barabara hii inayokwenda huko Kusini (Mtwara - Lindi) na inafika mpaka huko kwenye Mkoa wa Ruvuma kwa jiografia yake.

Mheshimiwa Spika, na ninaendelea kukumbuka na kurejea maelezo ya Serikali na hasa viongozi wa juu ambavyo walikuwa na concern kubwa na barabara hiyo na hiki ambacho Waheshimiwa Wabunge wanakieleza kwa sasa ndani ya Bunge lako tukufu, ninaomba sana jambo hili tulichukue turudi ndani ya Serikali, tukafanye majadiliano na kwenda kufanya tathmini ya kina ya kujua nini kinachofanyika na hii itatusaidia kuokoa fedha za wananchi wa Tanzania walipa kodi katika kutekeleza miradi ambayo hailingani na thamani ya fedha na uhalisia unaotakiwa katika eneo husika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hapa hatuwezi kupata nafasi ya kufanya haya majadiliano ya kina na kutoa tathimini ya uhakika naomba uridhie tulichukue Serikali na tukalifanyie kazi. (Makofi)