Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. HASSAN E. MASALA) aliuliza:- Redio ya Taifa (TBC) haisikiki Wilayani Nachingwea, pamoja na kuwepo kituo cha kurusha matangazo katika eneo la Stesheni. (a) Je, ni tatizo gani linasababisha kutosikika kwa Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukifanyia ukarabati kituo cha kurushia matangazo Nachingwea ambacho pia ni chanzo cha ajira kwa wakazi wa jirani na kituo?

Supplementary Question 1

MHE.HAMIDA M. ABDALLA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri, kwa majibu yake yenye matumaini.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mikoa hii ya Lindi tuna majina mengi sana, tunaitwa Mikoa ambayo imesahaulika, Mikoa iliyokuwa pembezoni, Mikoa ya Kusini. Tunapata hofu sana tunapokosa matangazo na matangazo kusikika katika eneo la mjini tu, wakati Wilaya ya Nachingwea ina kata 34, na wanahitaji kupata matangazo. Ningependa Mheshimiwa Waziri atuthibitishie wananchi wa Wilaya ya Nachingwea ni lini atapata fedha ili kwenda kujenga mtambo huu?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimthibitishie tu kwamba tumeweka kipaumbele kwenye Mikoa ambayo iko pembezoni ambayo kwa kweli usikivu wa vituo vyetu vya Taifa umekuwa mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi nimefanya ziara kwenye Mikoa 13 ya pembezoni lakini kwa Mkoa wa Lindi ambapo mimi natoka na Waziri Mkuu anatoka, na sisi ni waathirika wa tatizo hili, nataka nikuhakikishie kwamba imefanyika tathimini na hivi tunavyoongea juzi Katibu Mkuu wa Wizara yangu ametoka huko pamoja na Mkurugenzi wa TBC wakiangalia namna tunaweza tukaanza hiyo kasi ya uboreshaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tu nikumbushe kwamba juzi Waheshimiwa Wabunge wamepitisha bajeti ya Wizara yangu na moja ya eneo ambalo tunawekeza kwa nguvu kubwa ni kuhakikisha tunaongeza usikivu. Wakati wa bajeti tulieleza hapa kwamba zaidi ya Wilaya 81 usikivu wa redio yetu hausikiki, kwa hiyo katika mipango yetu tutakwenda awamu kwa awamu na kipaumbele tutatoa kwa ile Mikoa ya mipakani na Mikoa inayoitwa ya pembezoni.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. HASSAN E. MASALA) aliuliza:- Redio ya Taifa (TBC) haisikiki Wilayani Nachingwea, pamoja na kuwepo kituo cha kurusha matangazo katika eneo la Stesheni. (a) Je, ni tatizo gani linasababisha kutosikika kwa Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukifanyia ukarabati kituo cha kurushia matangazo Nachingwea ambacho pia ni chanzo cha ajira kwa wakazi wa jirani na kituo?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa redio ya Taifa (TBC)haipatikani kabisa katika maeneo ya Lushoto hasa maeneo ya Makanya, Mlolo, Mlalo, Lushoto na Bumbuli.
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mitambo hiyo ili wananchi wa Wilaya ya Lushoto waweze kupata taarifa za nchi kama wananchi wengine?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamida, bahati nzuri kwenye hotuba yangu ya bajeti hapa tuliorodhesha Wilaya ambazo tutaboresha usikivu wake na Wilaya anayotoka Mheshimiwa Mbunge ni katika Wilaya tulizozitaja kabisa kwenye hotuba ya bajeti tuliyoiwasilisha hapa Bungeni.
Kwa hiyo nataka nikuhakikishie kwamba tathimini imekamilika, sasa kwa kuwa mmepitisha jana Finance Bill hapa fedha zitaanza kutoka na tutaweka kipaumbele kwenye eneo lako. Nikupongeze kwa kazi nzuri unayofanya kuwatetea wananchi wa Jimbo lako.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. HASSAN E. MASALA) aliuliza:- Redio ya Taifa (TBC) haisikiki Wilayani Nachingwea, pamoja na kuwepo kituo cha kurusha matangazo katika eneo la Stesheni. (a) Je, ni tatizo gani linasababisha kutosikika kwa Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukifanyia ukarabati kituo cha kurushia matangazo Nachingwea ambacho pia ni chanzo cha ajira kwa wakazi wa jirani na kituo?

Supplementary Question 3

MHE. MASHIMBA M.NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile pia usikivu wa Redio ya Taifa ni dhaifu sana kwenye Mkoa wa Simiyu na kwa vile hakuna mwakilishi Mkoa wa Simiyu anayewakilisha TBC wala Redio ya Taifa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwa na mwakilishi Mkoani na pia kuboresha usikivu huo?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mikoa ambayo nilitembelea mwanzoni ni pamoja na Mkoa wa Simiyu na nilipofika ni kweli nilikuta tatizo la TBC kutokuwa na mwakilishi. Hii ilitokana na kwamba Mkoa huu ulikuwa ni sehemu ya Mkoa wa Shinyanga. Kwa hiyo, TBC ilikuwa na mwakilishi pale Shinyanga, ulipopatikana Mkoa mpya taratibu zilikuwa zinafanyika za kupata mwakilishi pale, bahati mbaya taratibu hizo zilikuwa zinakwenda taratibu. Nilipotoka pale tumeagiza na taratibu hizo zimekamilika na sasa Mkoa wa Simiyu utakuwa na mwakilishi wa TBC na hivyo kazi za TBC zitafanyika vizuri katika Mkoa wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado liko tatizo la usikivu kama ilivyo katika mikoa mingine ambayo inakabiliwana tatizo hilo na Mkoa wa Simiyu ni katika mikoa ya kipaumbele katika uboreshaji wa matangazo ya Shirika la Utangazaji la Taifa.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. HASSAN E. MASALA) aliuliza:- Redio ya Taifa (TBC) haisikiki Wilayani Nachingwea, pamoja na kuwepo kituo cha kurusha matangazo katika eneo la Stesheni. (a) Je, ni tatizo gani linasababisha kutosikika kwa Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukifanyia ukarabati kituo cha kurushia matangazo Nachingwea ambacho pia ni chanzo cha ajira kwa wakazi wa jirani na kituo?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Waziri ametembelea mpaka Wilayani kwangu Nkasi kule na kujionea mwenyewe jinsi matatizo ya mawasiliano ya Redio TBC hayafiki kule kwetu. Ni lini sasa bataweka mkazo ili watu wanaokaa mwambao mwa Ziwa Tanganyika waache kutegemea matangazo kutoka DRC Congo?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba katika Mikoa michache ambayo nimeitembelea ni pamoja na Mkoa wa Rukwa na Jimboni kwake Nkasi na nimpongeze kwa juhudi walizozifanya Halmashauri ya Wilaya Nkasi kwa kuanzisha redio yao na inafanya vizuri sana. Ni kweli pia kwamba usikivu wa Shirika la Utangazaji la Taifa kwa Wilaya ya Nkasi ni mbovu na baadhi ya maeneo yakiwemo ya Kabwe na maeneo mengine kwa kwa kweli wanasikiliza matangazo kutoka nchi jirani ya Congo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema tumeweka mkazo mkubwa kuhakikisha mikoa hii ya pembezoni tunaimarisha usikivu wa Shirika letu la Utangazaji la Taifa ili wananchi wetu waache kusikiliza redio za nchi jirani ikiwezekana watu wa nchi jirani wasikilize redio yetu na Shirika letu la Utangazaji wa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie katika maeneo yote niliyotembelea kwa bahati nzuri, baada ya ziara yangu Mkurugenzi wa TBC Dkt. Rioba amekwenda huko nilikopita, na kuhakikisha kwamba yale niliyoyaagiza yanatekelezwa; na nichukue nafasi hii kumpongeza Mkurugenzi wa TBC kwa kazi nzuri anayofanya, ya kulibadilisha Shirika letu la Utangazaji na mimi naamini kwamba kwa kasi yake mambo yatakwenda vizuri.