Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 50 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 427 2016-06-24

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. HASSAN E. MASALA) aliuliza:-
Redio ya Taifa (TBC) haisikiki Wilayani Nachingwea, pamoja na kuwepo kituo cha kurusha matangazo katika eneo la Stesheni.
(a) Je, ni tatizo gani linasababisha kutosikika kwa Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kukifanyia ukarabati kituo cha kurushia matangazo Nachingwea ambacho pia ni chanzo cha ajira kwa wakazi wa jirani na kituo?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nachingwea lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, matangazo ya Redio ya Taifa katika Jimbo la Nachingwea yalikuwa yakisikika maeneo yote ya Wilaya ya Nachingwea na Mikoa ya Kusini kwa ujumla kupitia mtambo wa masafa ya kati (medium wave) wa kilowati 100 ambao tangu tarehe 01/01/2012 haufanyi kazi kutokana na uchakavu. Kwa hivi sasa eneo la Nachingwea Mjini ndilo linalopata matangazo ya Taifa kwa kutumia mitambo miwili midogo ya redio, FM ya watt 230 (TBC- FM) na watt 100 TBC-Taifa, ambayo imefungwa katika kituo cha redio kilichopo eneo la Songambele.
Mheshimiwa Naibu Spika, nia ya Serikali, ni kufunga mitambo mpya na ya kisasa ya FM yenye nguvu kubwa ya kilowati mbili pale fedha zitakapopatikana.
Mtambo huo utakuwa na uwezo wa kurusha matangazo yatakayowafika wananchi sehemu mbalimbali. Ufungwaji wa mitambo hiyo utaenda sambamba na ukarabati wa majengo ya mitambo, Ofisi na miundombinu mbalimbali ya kituo cha Nachingwea.