Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Je, ni lini Mradi mkubwa wa Maji wa Ziwa Victoria kutoka Busega mpaka Itilima kupitia Bariadi utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali tayari imemaliza kushauriana na wenzetu wa KFW na tayari kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022 Serikali imetenga bilioni 19 za ndani kwa ajili ya kuanza mradi huu. Je, ni kiasi gani kimetengwa kwa kutoka kwa hawa marafiki zetu wa KFW kwa ajili ya mradi huu kwa mwaka wa fedha 2021/2022?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa, miradi mingi ya maji imekuwa ikitengenezwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu tu na Mkoa wetu wa Simiyu wananchi walio wengi ni wakulima na wafugaji. Je, Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Mkoa wa Simiyu kwamba, mradi huu utaenda kuwasaidia katika zoezi zima la umwagiliaji na matumizi ya mifugo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Simon Lusengekile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anahitaji kufahamu ni kiasi gani kimetengwa na hawa wenzetu wa Serikali ya Ujerumani:-

Mheshimiwa Spika, kwa majibu ya rahisi ni kwamba, sisi tumetenga hiyo milioni 19 ambavyo imesomeka kwenye bajeti yetu na kwa Serikali ya Ujerumani wametenga bilioni 55 kwa ajili ya mradi huu. Na huu mradi ni mradi mkubwa ambao utakwenda kugharimu zaidi ya bilioni 444, fedha za ndani zitakazotumika zitakuwa ni bilioni 124 na fedha za KFW 320.

Mheshimiwa Spika, kwa suala la kuzingatia umwagiliaji na ufugaji, sisi kama Wizara tumezingatia na tumeweza kuona kwamba tunaenda kuhakikisha kukabiliana na mabadiliko ya tabia-nchi katika Mkoa wa Simiyu. Na shughuli kubwa ambazo zitaendelea kufanyika ni ujenzi wa mabwawa ambayo yatatumika katika umwagiliaji, lakini vilevile malambo katika namna ambavyo tutaendelea kupata fedha katika miaka ya fedha ya mwaka 2021/2022 pia malambo kwa ajili ya mifugo yatajengwa.