Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 38 Water and Irrigation Wizara ya Maji 320 2021-05-27

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:-

Je, ni lini Mradi mkubwa wa Maji wa Ziwa Victoria kutoka Busega mpaka Itilima kupitia Bariadi utaanza kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songwe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la KFW la Serikali ya Ujerumani imekamilisha taratibu za kupatikana kwa wataalam washauri ambao watasimamia utekelezaji wa mradi huu mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka Mkoa wa Simiyu. Mradi huu unahusisha ujenzi wa bomba kuu kilomita 195, matenki 8 yenye ujazo wa lita milioni 11.9 na mabomba ya usambazaji kilomita 49.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa mradi unatarajia kuanza mwezi Agosti 2021 na miji mikuu ya Wilaya itakayonufaika ni Busega, Bariadi, Itilima, Maswa, Meatu na vijiji vilivyoko pembezoni mwa bomba kuu umbali wa kilomita 12 kila upande. Mradi umepangwa kutekelezwa kwa miaka minne.