Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Jeshi la Polisi linao uwezo wa kukomesha tatizo sugu la ubakaji na ulawiti kwa watoto wadogo nchini:- Je, ni kwa nini Serikali isiunde Kikosi Maalum cha kuwashughulikia watu wanaojihusisha na vitendo vya ubakaji na ulawiti?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuongeza maswali mawili ya ziada. Swali langu la kwanza, nataka nijue kwa kuwa, suala la ubakaji na ulawiti na unyanyasaji kwa watoto haliko Tanzania pekee, lipo katika nchi mbalimbali. Nilitaka kujua Serikali inashirikiana na mashirika gani, ili kuhakikisha suala hili linakomeshwa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa, kuna maafisa wa madawati katika maeneo kadhaa, ili kusaidia kupambana na masuala ya ulawiti, ubakaji na unyanyasaji kwa watoto, nilitaka kujua wanawawezeshaje maafisa wale, ili waepukane na rushwa, lakini pia waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, anataka kujua ni mashirika gani ya kimataifa au mashirika gani ambayo tunashirikiananayo katika kupambana na jambo hili. Kwa kweli, niseme tu kwamba, yapo mashirika mengi ambayo tunashirikiananayo. Yapo ya ndani na nje ya nchi ambayo tunashirikiananayo katika kupambana dhidi ya matukio haya ya uhalifu, hasa ya udalilishaji wa kijinsia. Kwa upande wan je huko tuna mashirika kwa mfano ya UNICEF, kuna shirika La WHO (World Health Organization), tuna UN Women, tuna USAID, tuna Save the Children, hapa tuna akina taasisi zile zinazoshughulikia masuala ya kisheria. Kwa hiyo, kwa ufupi tuna taasisi nyingi ambazo tunashirikiana nazo katika kuhakikisha kwamba, tunapambana dhidi ya haya matukio ya udhalilishaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu vipi tunawawezesha hawa maafisa wa madawati; maafisa wa madawati tuna mambo mengi. La kwanza tuna mfumo maalum ambao upo kwa ajili ya uwezeshaji na ufuatiliaji wa matukio ya udhalilishaji, lakini pia tumekuwa tunawapa elimu ya kisheria, tunawapa elimu ya protections, tunawapa elimu ya kijamii. Elimu ambazo zinawasaidia wao kuweza kuchukua hatua pale tukio linapotokea, lakini zaidi tumeanzisha kwenye vituo pamoja na kwamba sio vyote, lakini vipo vituo ambavyo tumewawekea usafiri ambao huwa wanatumia kwa ajili ya kufuatilia hayo matukio mara tu yanapotokea. Nakushukuru.