Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 38 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 318 2021-05-27

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-

Jeshi la Polisi linao uwezo wa kukomesha tatizo sugu la ubakaji na ulawiti kwa watoto wadogo nchini:-

Je, ni kwa nini Serikali isiunde Kikosi Maalum cha kuwashughulikia watu wanaojihusisha na vitendo vya ubakaji na ulawiti?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kupambana na tatizo sugu la ubakaji na ulawiti Jeshi la Polisi limejiwekea mikakati thabiti inayohusisha ufuatiliaji wa vyanzo vya makosa na kuyatafutia ufumbuzi. Moja miongoni mwa mikakati hiyo ni kutoa elimu kwa kushirikisha jamii kupitia madawati ya unyanyasaji wa jinsia yaliyopo kwenye vituo vya polisi. Aidha, hutoa elimu ya mapambano dhidi ya makosa ya aina hii katika shule za msingi na sekondari, maadhimisho pia ya kitaifa na matamasha mbalimbali. Aidha, wale wote wanaobainika kutenda makosa hayo huchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Mheshimwa Spika, kwa sasa mikakakati ya jeshi la polisi inatosheleza kukabiliana na tatizo hilo bila ya kuhitaji kuanzishwa kwa kikosi maalum kwani yote ya jinai ikiwemo udhalilishaji yana adhabu zake kisheria. Aidha, makosa haya yanatendeka miongoni mwa jamii hivyo, ni lazima jamii nzima ishirikiane kuyapinga na kuyakataa kwa kutoa taarifa vituo vya polisi na kuwa tayari kwenda kutoa ushahidi mahakamani, ili adhabu stahiki zitolewe kwa wahalifu hao, ahsante.