Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kurasimisha Bandari ya Mbweni kuwa Bandari ndogo?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, bandari hiyo sasa imesharasimisha na ninaipongeza sana Serikali: Je, Serikali sasa ina mpango gani wa muda mfupi kuboresha eneo hilo ili liweze kufikika?

Swali la pili; kwa kuwa wanawake wa Kata ya Mbweni ni wadau wakuu katika eneo hilo la bandari: Je, Serikali ina mpango gani ya kuwatengea eneo mahususi kabisa ya kufanya shughuli za ujasiliamali ili nao waweze kufahidika na fursa hiyo ya bandari? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya muda siyo mrefu sana tutatembelea eneo hilo. Anasema kuna shida ya barabara kwamba eneo halifikiki; tutarekebisha miundombinu ili waweze kupata huduma nzuri pale.

Mheshimiwa Spika, swali la pili amewasemea akina mama wa nchi hii na hasa Mkoa wa Dar es Salaam maeneo ya Mbweni; naomba niseme tumepokea wazo hili nzuri na jema, tutalifanyia kazi akina mama wapate sehemu maalum ya kufanya shughuli zao katika Bandari ya Mbweni. Ahsante.