Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 35 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 288 2021-05-24

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kurasimisha Bandari ya Mbweni kuwa Bandari ndogo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbuge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imekamilisha kazi ya kutambua Bandari bubu zote zilizo katika mwambao wa Bahari ya Hindi ikiwemo bandari ndogo ya Mbweni kwa ajili ya kurasimishwa kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania kwa kushirikaina na Manispaa ya Kinondoni, zipo katika hatua ya kutambua mipaka ya eneo la bandari hiyo kwa upande wa bahari na nchi kavu ili kuweka miundombinu rafiki kama vile maegesho ya majahazi, barabara, ofisi, choo, maji, umeme na ghala la kuhifadhia mizigo.

Mheshimiwa Spika, tangu mwezi Februari, 2020, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania imepeleka wafanyakazi na mashine za POS katika bandari ndogo ya Mbweni ili kusimamia shughuli za kibandari na kukusanya mapato. Katika miezi tisa ya mwaka wa fedha 2020/2021 (Julai 2020 hadi Machi 2021), TPA imeweza kukusanya kiasi cha shilingi milioni 117. Mapato hayo yanatarajiwa kuongezeka baada ya kuirasimisha bandari hiyo na kuiwekea miundombinu muhimu.

Mheshimiwa Spika, kwa hivi sasa ipo katika hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi Mshauri ambaye pamoja na mambo mengine, atafanya usanifu katika Bandari za Mbweni na Kunduchi na kushauri aina ya uwekezaji wa miundombinu itakayofaa katika bandari hiyo. Ahsante.