Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume, akina mama na watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Frelimo katika Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini niseme kwamba Hospitali ya Frelimo ilijengwa ili kupunguza msongamano mkubwa sana uliopo katika Hospitali yetu ya Mkoa na mpaka sasa hivi tunashukuru kwamba tumeweza kupata milioni 500, lakini hakuna hata wodi moja toka mwaka 2012 imeanzishwa, lakini pia tushukuru kwa hizi shilingi milioni 400 ambazo tumepewa kwa ajili ya kujenga majengo ya maabara na uchunguzi.

Sasa ni lini Serikali italeta vifaa kama vya X-Ray, MRA, CT Scan ili sasa wananchi wa Iringa wasiendelee kwenda kwenye Hospitali ya Mkoa?

Mheshimiwa Naibu Spika, Swali langu la pili, Sera ya Serikali ni kujenga vituo vya afya kila kata. Lakini Manispaa yetu ya Iringa ina kata 18 na ina vituo viwili tu vya Ngome na Ipogolo, vituo ambayo kwa kweli ni vichakavu mno na havijawahi kufanyiwa ukarabati wowote toka vimeanzishwa. Na tulitegemea kwamba hivi vituo…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ritta Kabati uliza swali.

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Kuna population karibu ya watu laki mbili.

Je, ni lini Serikali sasa hivi itaboresha hivi vituo vya afya ili viweze kufanya huduma ya upasuaji ili kupunguza msongamano mkubwa uliopo katika Hospitali yetu ya Mkoa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru kwa kutambua kwamba Serikali imeendelea kuwekeza fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Hospitali hii ya Manispaa ya Iringa - Frelimo inatoa huduma na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie kwamba, kama ambavyo tumeweka katika mipango yetu katika mwaka wa fedha ujao tutaendelea kutenga fedha kwa awamu ili kuhakikisha wodi zote katika hospitali ile zinajengwa, zinanakamilika ili ziweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi wa Manispaa ya Iringa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimhakikishie kwamba vifaa tiba ni moja ya kipaumbele cha Serikali na ndio maana katika bajeti yetu 2021/2022 tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 14 kwa ajili ya kununua vifaa tiba katika vituo vyetu na hospitali zetu. Kwa hiyo, nimuhakikishie hospitali hii pia itapewa kipaumbele kuhakikisha kwamba tunakwenda kupeleka vifaa tiba katika hospitali ile.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tatu kuhusiana na vituo vya afya tutaendelea kujenga na katika mwaka wa fedha ujao Manispaa ya Iringa ni moja ya Manispaa ambazo zitajengewa vituo vya afya.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume, akina mama na watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Frelimo katika Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, hali inayoonekana Manispaa ya Iringa yaani inafanana moja kwa moja na hali iliyopo kwenye Halmashauri ya Masasi. Kwa sababu ni kata 18 kama ilivyo, lakini hali kadhalika vituo vya afya viwili na hali ni mbaya kabisa.

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Mchungahela.

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu je, ni lini Serikali itatuwezesha kuwa na vituo vya afya zaidi, maana yake vituo viwili vya afya ni vichache?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela, Mbunge wa Jimbo la Lulindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri ya Masasi Vijijini katika mwaka wa fedha kuna fedha ambazo zimetengwa katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya kujenga vituo vya afya. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie kambwa pamoja na bajeti yetu 2021/2022 kutenga fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya kwa mapato ya ndani lakini pia kwa fedha za Serikali Kuu tutaendelea kutenga fedha kuhakikisha jimbo hilo pia linapata vituo vya afya.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume, akina mama na watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Frelimo katika Manispaa ya Iringa?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa swali la nyongeza.

Kama ulivyosimamia hospitali ya Makandana na kupata wodi ya wanawake bado tunashida ya x-ray wananchi wanaambiwa waende hospitali ya Igogwe. Ni lini Serikali itatupatia x-ray mpya katika hospitali ya Makandana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hospitali ya Halmashauri ya Rungwe maarufu kama Makandana ina tatizo la x-ray pamoja na juhudi za Serikali za kuboresha miundombinu mingine, kipaumbele pia ni kupeleka vifaa tiba zikiwemo x-ray. Na katika mipango ya fedha ya miaka ijayo tutahakikisha pia hasa mwaka ujao katika mgao wa x-ray lakini na vifaa tiba vingine tunaipa kipaumbele Halmashauri ya Rungwe kwa maana ya Hospitali ya Makandana.