Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mbalizi – Shigamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Pia nashukuru sana kwa Mheshimiwa Naibu Waziri na hata pacha wake kwenye Wizara hiyo, wanaifahamu sana jiografia ya Wilaya ya Mbeya na hasa Mbalizi. Swali la kwanza, ahadi nyingi zimetolewa, hata wewe utakumbuka kuwa, eneo la miteremko ya Iwambi – Mbalizi lina ajali nyingi na zinaendelea. Mheshimiwa Rais wa sasa tarehe 15 alipotembelea na kuwapa pole wananchi wa Mbalizi kwa ajali mbaya iliyoua watu zaidi ya 20, aliahidi ujenzi wa Barabara ya By-pass ya Uyole – Songwe na By-pass ya Mbalizi – Iwambi. Sasa ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; bandari kwa muda mrefu walitwaa eneo la Inyala kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu, lakini kwa miaka mingi sasa hawajaweza kuwalipa wananchi na wananchi hawafanyi shughuli zozote za uzalishaji. Sasa ni lini Wizara itaipa nafasi na kuiamuru Mamlaka ya Bandari walipe fidia kwa wananchi wa Inyala, Mbeya? Nashukuru sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ni kweli kwamba, Mheshimiwa Rais, Mama Samia, alipita katika eneo ambalo ametaja na akatoa maelekezo. Bahati nzuri tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa kupitisha bajeti yetu jana na miongoni mwa fedha ambazo zimetengwa ni pamoja na malipo ya Barabara hii ya By-pass pale Uyole – Songwe. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na amani tutakapoanza utekelezaji wa bajeti hii hili eneo tutazingatia maelekezo ya kiongozi mkuu wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, anazungumza habari ya fidia ya Bandari Kavu, Inyala. Miongoni mwa maeneo muhimu ambayo tumepanga kujenga Bandari Kavu ni pamoja na Inyala, ambayo itahudumia ukanda wa Nyanda za Juu Kusini. Kwa hiyo, kwa sababu anasema kwamba, kuna shida pia ya mawasiliano naomba nimhakikishie kwamba, shida hiyo itamalizika fidia iweze kulipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukubaliane baada ya maswali na majibu tuongee na Mheshimiwa Mbunge tupate exactly hasa malalamiko yako wapi, ili utekelezaji wa jambo hili ufanyike, wananchi walipwe fidia zao, wafanye shughuli za maendeleo, lakini pia bandari hii ijengwe na Serikali iweze kumiliki eneo hili ili na kupunguza migogoro kati ya wananchi na Serikali yao pendwa ya Chama Cha Mapinduzi.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mbalizi – Shigamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwenye majibu ya Waziri, Barabara hii ya Karatu – Mbulu – Haidom – Sibiti, lakini kwenye Ilani kuna barabara hii ya Lalago – Mwanhuzi – Kolandoto – Matala – Karatu. Sasa kwenye majibu ya Waziri amesema kilometa 25 kupitia Barabara ya Karatu – Mbulu, sasa ni lini Barabara ya Lalago
– Kolandoto – Mwanhuzi – Matala – Karatu itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara zote mbili ambazo amezitaja ziko kwenye bajeti lakini pia zinajengwa kwa awamu kwa Kulandoto na maeneo mengine ambayo yametajwa tutaenda hatua kwa hatua kadri ambavyo tutapata fedha. Lakini bahati nzuri kwamba ipo kwenye bajeti, pia vipande baadhi vimeanza kujengwa kwa mwaka wa fedha huu ambao unaendelea, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mbalizi – Shigamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali, barabara ya kutoka Makutano, Butiama Nyamswa na Sanzati ni barabara imejengwa kwa muda mrefu sana mkataba wake ulikuwa miaka miwili sasa ni miaka minane toka imeanza kujengwa kama ni bajeti ilikuwa na bajeti ya shilingi bilioni 46 sasa inaenda mpaka Bilioni 50 ni lini sasa hiyo barabara itakamilika? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI – (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara hii imechukua muda mrefu ni miongoni mwa miradi ya barabara ambayo ilikuwa na mkwamo na Mheshimiwa Mbunge anajua kwamba changamoto zimetatuliwa barabara inaendelea kujengwa na kazi itakwisha matarajio mwaka huu kabla haujakwisha hadi mwaka ujao itakuwa imeshakamilika barabara hii, na tumepanga baada ya Bunge kukamilika tutaenda kutembelea barabara ile ili kuona hali halisi katika eneo la ujenzi. Ahsante.