Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 31 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 268 2021-05-19

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mbalizi – Shigamba kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Mbalizi – Shigamba yenye urefu wa kilometa 52.2 ni barabara ya mkoa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Songwe kupitia Wilaya ya Mbeya Vijijini na Wilaya ya Ileje. Barabara hii ni ya changarawe na udongo ambayo hupita sehemu zenye miinuko na miteremko mikali, hivyo kupitika kwa shida wakati wa mvua kutokana na utelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa katika Kampeni za Uchaguzi wa mwaka 2020, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, alipokuwa akiongea na wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi aliahidi kuijenga Barabara ya Mbalizi – Shigamba kwa kiwango cha lami. Hata hivyo, utekelezaji wa ahadi za Viongozi, ikiwemo ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Mbalizi – Shigamba hufanyika kwa awamu kulingana na upatikanji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inatafuta fedha ili kuanza kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hiyo ili ijengwe kwa kiwango cha lami. Wakati Serikali inatafuta fedha za kuanza taratibu za ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali kwa kiwango cha changarawe ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Ahsante.