Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka Kivuko katika Mto Ruvuvu ili kuunganisha Vijiji vya Mayenzi na Kanyinya vilivyopo Wilayani Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Mto Ruvuvu una tabia ya kujaa, hali inayoweza kusababisha kivuko hiki kutofanya kazi, hasa nyakati za masika; na kwa kuwa vivuko hivi vina tabia pia ya kupata hitilafu, hali ambayo inasababisha huduma ya kuvusha wananchi isiwepo. Swali la kwanza; je, Serikali iko tayari kutuletea mtumbwi wa kisasa ili uweze kutoa huduma pindi ambapo kivuko kitakuwa hakiwezi kufanya kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuambatana na mimi twende kwenye Jimbo la Ngara akashuhudie changamoto zetu za vivuko pamoja na miundombinu mingine, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza kwa swali lake zuri kwa sababu anatu-alert kwamba tunapojenga vivuko tuweke pia na mitumbwi kama backup ikitokea tatizo tuweze kupata huduma katika maeneo hayo. Naomba nimuelekeze Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi atume wataalam wetu waende katika eneo hili la Mto Ruvuvu akafanye tathmini tujue aina ya mtumbwi na gharama zake ili tuweze kupeleka huduma hii muhimu katika eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ndaisaba kwamba kwakuwa ni mjukuu wangu nitaenda pale Kagera kutembelea Ngara katika eneo hili baada ya Bunge hili kumaliza Bunge la Bajeti, ahsante.