Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 30 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 260 2021-05-18

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Kivuko katika Mto Ruvuvu ili kuunganisha Vijiji vya Mayenzi na Kanyinya vilivyopo Wilayani Ngara?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepanga kuendelea kuboresha huduma za usafiri kwa njia ya maji ikiwa ni pamoja na kuunganisha maeneo yenye mahitaji ya vivuko ikiwemo Mayenzi na Kanyinya kila inapopata fedha. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Sekta ya Ujenzi, ilitenga fedha kwa ajili ya kujenga maegesho ya Mayenzi na Kanyinya, ili iweze kupeleka kivuko ambacho kitaunganisha wananchi wa maeneo hayo. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maegesho hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) uko kwenye hatua za ununuzi wa kumpata mkandarasi wa kufanya ujenzi wa maegesho ya kivuko hicho na mkandarasi wa kufanya ukarabati huo chenye uwezo wa kubeba abiria 60 na magari mawili ambacho hapo awali kilikuwa kinafanya kazi eneo la Rusumo
– Nyakiziba, yaani MV Ruvuvu ya zamani, ambacho kwa sasa kimeegeshwa katika Mto Ruvuvu. Baada ya ukarabati huo kukamilika, kitatoa huduma kwenye eneo la kati ya Mayenzi hadi Kanyinya. Ahsante.