Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Idofi watalipwa fidia baada ya maeneo yao kuchukuliwa na Serikali kwa ajili ya kujenga Mradi wa Idofi One Stop Centre?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa wananchi wale wamesubiri kulipwa fidia kwa muda mrefu; na kwa kuwa, hawawezi kuendeleza kufanya shughuli yoyote katika maeneo yaliyozuiliwa, wanapata shida katika nyumba zao, hawawezi kuongeza kitu: Je, sasa Serikali imejipangaje; ni lini itawalipa fedha zilizobakia ili waweze kupisha ujenzi wa mradi huu wa One Stop Centre? (Makofi)

Swali la pili; kwa sababu fedha za kujenga mradi huu zilishatengwa na zipo; nilipofuatilia fedha hizi zipo: sasa ni lini mradi huu ambao una manufaa makubwa kwa wananchi wa Makambako utaanza kujengwa? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia fidia kwa wananchi wake wa Jimbo lake la Makambako.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mradi huu una maslahi makubwa na mapana kwa nchi yetu na kwa uchumi wa nchi yetu hasa kwa wasafirishaji upande wa SADC na East Africa Community, hata hivyo, fedha hizi ni za World Bank. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imelipa uzito, litafanyiwa kazi mapema iwezekanavyo tulipe fidia kwa wananchi hawa ili wapishe kazi ya ujenzi ifanyike na huduma ya uchukuzi iweze kuboreshwa katika Wizara yetu ya Ujenzi na Uchukuzi. Ahsante.