Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 252 2021-05-17

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-

Je, ni lini Wananchi wa Idofi watalipwa fidia baada ya maeneo yao kuchukuliwa na Serikali kwa ajili ya kujenga Mradi wa Idofi One Stop Centre?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza miradi ya ujenzi wa vituo vya pamoja vya ukaguzi wa magari ya mizigo (One Stop Inspection Station) katika shoroba mbalimbali za barabara nchini, ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi Makambako katika eneo la Idofi.

Lengo la ujenzi wa vituo hivyo ni kupunguza vikwazo visivyo vya kiforodha kwa wasafirishaji wa nchi za SADC na EAC wanaotumia barabara zetu. Vituo hivyo vitakapokamilika vitakuwa na Ofisi ya Polisi, TRA, Afya, Uhamiaji na Vituo vya Mizani katika eneo moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kituo cha Makambako hadi kufikia Aprili, 2021 jumla ya shilingi 870,182,049 zimelipwa kwa wananchi 39 kati ya 275 wanaopisha ujenzi wa mradi huo. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta jumla ya shilingi 3,758,635,767 ili kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi 236 waliosalia. Ahsante.