Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa makubwa ambayo yatahifadhi maji ya mvua ili yaweze kutumika kwa shughuli za kibinadamu, kilimo na mifugo katika Mkoa wa Dodoma ambao umekuwa haupati mvua za kutosha?

Supplementary Question 1

MHE. KENETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, swali langu la msingi ilikuwa ni kwamba Mkoa wa Dodoma unapata mvua kidogo lakini kumekuwa na upotevu mkubwa wa maji kipindi mvua inavyokuwa inanyesha.

Lengo la swali langu ni je, Serikali ina programu gani mahsusi, acha hii ya kudonoa donoa, programu mahsusi ya kuanza kukinga maji ambayo yanapotea kwa kiasi kikubwa kwa miaka nenda rudi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; tunajenga reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza. Lakini, mradi huu ni mkubwa unapita kwenye mabonde na mito mingi. Je, Serikali kupitia Wizara ya Fedha, Kilimo na Wizara ya Ujenzi haioni kwamba tuongeze sehemu ya mradi ule kwa ajili sasa ya kuweka mabwawa na kutengeneza upatikanaji wa maji kwa ajili ya kilimo badala ya fedha nyingi zinajenga kwenye reli lakini mradi ule hauna pact ambayo ingeweza kusaidia kwenye Sekta ya Kilimo. Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango mahsusi wa Serikali kutumia maji ya mvua kama nilivyoelekeza, tuna mpango wa kuchimba mabwawa ambayo yataweza kuvuna yale maji na yatasambazwa kwa wananchi wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kuhusiana na ujenzi wa reli ya kisasa. Pamoja na kwamba hii ni nje ya Wizara yangu nipende tu kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba reli hii ni ya thamani kubwa sana na ni ya manufaa makubwa kwa wananchi hivyo, kila suala lina mkakati wake na umuhimu wake. Masuala ya mabwawa kuongezwa, sisi kama Wizara ya Maji tutashughulikia. Licha ya kwamba mradi huo wa reli manufaa yake yataendelea kuzingatiwa. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa makubwa ambayo yatahifadhi maji ya mvua ili yaweze kutumika kwa shughuli za kibinadamu, kilimo na mifugo katika Mkoa wa Dodoma ambao umekuwa haupati mvua za kutosha?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Mbali na mkakati wa Serikali katika jibu lake la msingi la kuchimba mabwawa na marambo. Jimbo la Bunda Mjini limekuwa na changamoto sana ya ukarabati wa marambo.

Sasa ni lini Serikali mtatukarabati Rambo la Nyabehu, Kinyambwiga na Gushigwamara ili sasa wananchi wa maeneo hayo wapate huduma ya maji vile vile mifugo iweze kupata huduma ya maji. Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati wa mabwawa na marambo kwa ajili ya mifugo, sisi kama Wizara tunaendelea kukarabati awamu kwa awamu kadri fedha inavyopatikana. Hivyo, pia kwa suala hili la Bunda Mjini, Bwawa la Nyabehu, Kinyambwiga pamoja na hilo lingine yote yapo katika mkakati wa Serikali kuona kwamba yanarudi katika hali bora. Hivyo, nipende kukupongeza Mheshimiwa Esther kwa kufuatilia na uongeze ushirikiano na Mbunge wa Jimbo ili mambo yakae sawa zaidi. (Makofi)