Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Water and Irrigation Wizara ya Maji 248 2021-05-17

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENETH E. NOLLO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa makubwa ambayo yatahifadhi maji ya mvua ili yaweze kutumika kwa shughuli za kibinadamu, kilimo na mifugo katika Mkoa wa Dodoma ambao umekuwa haupati mvua za kutosha?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Keneth Ernest Nollo, Mbunge wa Jimbo la Bahi, kama ifuatavyo:-

Mheshmiwa Naibu Spika, katika jitihada za kuboresha huduma ya maji kwa wananchi wa Dodoma, katika mwaka 2020/2021, Serikali imekamilisha usanifu kwa ajili ya kukarabati Bwawa la Chikopelo lililopo umbali wa kilomita 70 kutoka Bahi Mjini ili kuongeza upatikanaji wa maji katika vijiji sita ikiwemo Mji wa Bahi na usanifu kwa ajili ya ujenzi wa bwawa la Kidoka litakalohudumia vijiji saba ikiwemo Mji wa Chemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati na ujenzi wa mabwawa hayo unatarajiwa kufanyika katika mwaka 2021/ 2022, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa malambo sita katika Vijiji vya Mpamwata, Uwekela, Kambia, Nyasa, Kolema Kuu, Kidoka na Palanga katika Wilaya za Bahi na Chemba.

Mheshmiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali ina mpango wa kujenga bwawa la kimkakati katika Kata ya Farkwa ambapo mpaka sasa usanifu umekamilika na ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaotakiwa kupisha eneo la mradi wa ujenzi wa bwawa hilo umefanyika kwa asilimia 99. Bwawa hilo lenye mita za ujazo milioni 470 linatarajiwa kujengwa kwa awamu kutegemea na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika kuboresha huduma ya maji katika Jiji la Dodoma, Serikali imechimba visima visima nane na kukarabati visima vitatu vya zamani. Kazi ya ufungaji wa miundombinu inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021.