Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwasaidia Wananchi wa Mji wa Itigi kuweza kuvuna maji katika Mbuga inayozunguka Mji huo?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali juu ya upatikanaji wa maji katika maeneo yetu hasa Mji wa Itigi ambapo mimi ndio Mwakilishi wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi hii ya kuvuna maji katika Mji wa Itigi, ni swali la pili nauliza katika Bunge hili, Bunge lililopita niliuliza swali kama hili. Majibu yalikuwa tunajiandaa, dalili inaonesha kwamba watafanya.

Je, ni lini sasa uvunaji huu utaenda kufanya katika Mji wa Itigi na maeneo ambayo umeyataja ya Kayui, Muhanga na Kaskazi kujenga mabwawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, Lakini swali la pili, nashukuru pia Serikali kwa kukamilisha mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Itiga ambao una manufaa makubwa kwa wananchi lakini unawatua akina mama ndoo kichwani. Lakini gharama za kuunganisha maji yale kwenda ndani ni gharama kubwa sana. kwa hiyo, mtu wa kijijini kwa shilingi 200,000 ni hela nyingi. Je, Serikali ipo tayari kupunguza gharama za uunganishaji maji ili wananchi wanufanike na mradi huu mkubwa ambao Mbunge wao amehangaika nao kuupata na wizara imesaidia? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, uvunaji huu wa maji tunautarajia kuutekeleza katika mwaka wa fedha ujao kwa maana mwaka 2021/2022. Mheshimiwa Mbunge ahadi hii imekuwa ikitolewa toka huko awali lakini kwa sasa hivi kama tulivyokuwa tumeendelea kuongea RUWASA imekuwa ni mkombozi, RUWASA imekuwa ni chachu ya mageuzi ya utekelezaji wa miradi ndani ya Wizara. Hivyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ili sasa linaingia kwenye utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na gharama za uunganishaji, hili nalo limekuwa ni tatizo sugu. Hata hivyo, kama tulivyomsikia Mheshimiwa Waziri wakati wa uwasilishaji wa bajeti, ni suala ambalo tayari lipo katika uangalizi mkubwa ambapo tunahitaji kuona wananchi wanaenda kupata nafuu kubwa katika uunganishwaji wa huduma ya maji sio tu katika Mji wa Manyoni bali kwa Tanzania nzima.