Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 228 2021-05-11

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwasaidia Wananchi wa Mji wa Itigi kuweza kuvuna maji katika Mbuga inayozunguka Mji huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Itigi ni miongoni mwa miji miwili iliyopo katika Wilaya ya Manyoni. Mji huu unakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 32,000. Serikali imeendelea kutekeleza ahadi iliyoitoa kwa kuwasaidia wananchi wa maeneo yanayozunguka Mji wa Itigi kuweza kuvuna maji ambapo imekamilisha utambuzi wa awali wa maeneo ambayo yanafaa kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa katika Mji wa Itigi na katika Kijiji cha Kayui, Kata ya Magandu, Kijiji cha Muhanga, Kata ya Ipande pamoja na Kjiji cha Kaskazi, Kata Kitaraka ambayo yameonekana yanafaa kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa. Katika mwaka wa fedha 2021/ 2022, Serikali itakamilisha usanifu wa kina na kuainisha ukubwa wa mabwawa yatakayojengwa kuanzia mwezi Januari, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika mwaka wa 2020/2021 katika kuimarisha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji wa Itigi Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji mkubwa unaohudumia vijiji sita vya Songambele, Mlowa, Majengo, Tambukareli, Zinginali na Itigi. Mradi huu umekamilika mwezi Disemba, 2020 na kugharimu shilingi bilioni
2.64. Mradi umewezesha upatikanaji wa maji katika Mji wa Itigi kufikia asilimia 80.