Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe hasa kwenye Idara za Afya, Elimu na Kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu haya ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna haja ya kukaa nae baadaye tuangalie hizi takwimu vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na majibu hayo ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, moja ya sababu kubwa ya upungufu wa watumishi kwenye Halmashauri za Vijijini kama ilivyo Halmashauri ya Korogwe au kama ilivyo kwenye Jimbo la Mlalo kule kwa ndugu yangu Shangazi, sababu kubwa ni kwamba watumishi wanaenda kule, wakipata ajira wanahama. TAMISEMI mmekuwa mkipitisha uhamisho wa watumishi wakati mwingine bila kuzingatia maoni ya wakurugenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kujua ni lini sasa TAMISEMI mtakubali kuzingatia maoni ya Wakurugenzi kutoa watumishi mbadala kabla ya kuwahamisha waliopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; wakati mwingine tunaweza kupunguza shida ya upungufu wa walimu kwa kusawazisha Ikama ndani ya halmashauri yenyewe. Kwa mfano Halmashauri ya Korogwe zaidi ya miaka mitatu kifungu cha moving allowance hakijawahi kupat afedha. Inasababisha ugumu katika kusawazisha Ikama ya watumishi ndani ya halmashauri yetu. Ni lini Serikali itakuwa tayari sasa kutoa fedha ya kutosha kwenye vifungu hivi vya uhamisho ili kuweza kusababisha Ikama ndani ya Halmashauri yenyewe? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tumekuwa na changamoto ya upungufu wa watumishi katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa ikiwemo Halmashauri ya Korogwe. Lakini kama ambavyo nimetangulia kutoa m ajibu ya msingi kwamba Serikali imeendelea kuweka jitihada za kutosha kuhakikisha kwamba tunaendelea kuongeza watumishi katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kweli tumekuwa na changamoto kubwa sana ya watumishi hasa wanaokuwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa maeneo ya vijijini kuomba uhamisho wengi wao wakiomba kuhamia mijini. Ofisi ya Rais TAMISEMI na Serikali kwa ujumla imeendelea kuhakikisha inazingatia Ikama katika maeneo ya vijijini na imeendelea kuhakikisha inasimamia kwa karibu uhamisho wa watumishi hasa kutoka vijijini kwenda mijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba si kweli kwamba TAMISEMI imekuwa kila siku inapitisha maombi ya uhamisho kwa watumishi wote wanaoomba. Mara kwa mara tumekuwa tunachuja sababu za msingi ambazo zinasababisha baadhi ya watumishi kukubali lakini watumishi walio wengi kutokukubaliwa kupata uhamisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili Serikali imeweka utaratibu sasa. Ofisi ya Rais TAMISEMI tutaenda kuzindua mfumo wa kielektroniki ambao sasa maombi ya uhamisho yatapitishwa kwa njia ya kielektroniki na yatawezesha sasa kuchuja kwa uhakika zaidi hamisho zote ambazo zinaombwa na itawezesha sana watumishi wetu katika maeneo ya vijijini kubakia kufanya kazi katika maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili tutakwenda kuwa na mikataba ya watumishi wanaoajiriwa. Watumishi wengi wamekuwa wakiajiriwa maeneo ya vijijini, wakifika na kupata cheque number wanaanza kufanya jitihada za kuhama. Sasa kabla ya kuajiriwa tutahakikisha tunakuwa na mikataba kwamba baada ya kupangiwa kwenye vituo hivyo ni lazima wakae angalau miaka mitatu au mitano kabla ya kuanza kuomba vibali vya uhamisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii itatuwezesha sana kuhakikisha watumishi wetu katika maeneo ya vijijini wanabaki na kutoa huduma ambazo zinakusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ugumu wa kusawazisha watumishi kwa maana ya ikama katika maeneo yetu, ni kweli na Serikali imeendelea kutenga fedha za matumizi mengineyo kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha kuhakikisha yale maeneo ambayo yana watumishi wengi lakini maeneo mengine yana watumishi wachache tuweze kufanya usambazaji wa ndani ya halmashauri. Hili pia tumeendelea kusisitiza Wakurugenzi katika Serikali za Mitaa kutenga bajeti za uhamisho wa ndani katika halmashauri zao ili waweze kuhakikisha mgawanyo wa watumishi ndani ya halmashauri unazingatia ikama na angalau unakuwa reasonable.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaendelea kutenga fedha kuhakikisha msambao huu pia unakuwa wenye tija zaidi. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe hasa kwenye Idara za Afya, Elimu na Kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa changamoto ya upungufu wa watumishi iliyoko Wilaya ya Korogwe ni sawa sawa kabisa na iliyoko Jimbo la Babati Vijijini hasa Sekta za Afya na Elimu. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hili la watumishi hawa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna upungufu wa watumishi lakini kama ambavyo nimetangulia kusema kwenye jibu la msingi, Serikali imeendelea kutenga ikama kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaendelea kuandaa na kuomba vibali vya ajira kila Mwaka wa Fedha ili kuendelea kuongeza idadi ya watumishi katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Kwa hivyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Baran kwamba katika Wilaya ya Babati pia tutahakikisha tunaipa kipaumbele katika ajira za Mwaka wa Fedha ujao ili angalau tuendelee kuboresha idadi ya watumishi katika halmashauri hiyo.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe hasa kwenye Idara za Afya, Elimu na Kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa nafasi. Wilaya ya Misenyi ni Wilaya yenye Kata 20. Inavyo vituo vya afya viwili ambavyo havina watumishi kabisa pamoja na Idara za Elimu na Kilimo. Je, ni lini Serikali itaweza kutupatia watumishi wa kutosha ili watoe huduma nzuri kwa wananchi wa Wilaya ya Misenyi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao 2021/2022 Serikali na Ofisi ya Rais – TAMISEMI tumeomba vibali vya ajira takribani 12,000 kwa ajili ya watumishi wa kada mbalimbali katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa na hivyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Kyombo kwamba katika mgawanyo wa watumishi katika Mwaka ujao wa fedha tutahakikisha tunaitazama Halmashauri ya Misenyi kwa jicho la karibu ili tuendelee kuboresha huduma za afya katika vituo hivi ambavyo havina watumishi lakini pia katika kada nyingine katika halmashauri hiyo na kote nchini kwa ujumla wake.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe hasa kwenye Idara za Afya, Elimu na Kilimo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba niulize hivi, Je, Wizara ya TAMISEMI haioni umuhimu wa kuweka maafisa masoko kwenye halmashauri zetu. Tunajua kwamba tatizo kubwa kwenye halmashauri ni ukosefu wa masoko. Watu hawajaunganishwa na masoko, sasa tungekuwa na maafisa hawa wangetusaidia sana. Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika uendeshaji wa shughuli za masoko katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Serikali imeweka utaratibu ambao pamoja na wakuu wa idara wengine, wakuu wa idara ya fedha na biashara kuna maafisa biashara katika halmashauri zetu ambao kimsingi wanafanya kazi kwa karibu ambazo zinafanana sana na Maafisa Masoko.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo tunaendelea kuhakikisha kwamba tunaboresha mfumo huo kuhakikisha kwamba wale maafisa biashara ambao wanasimamia masoko na shughuli nyingine zote za biashara katika halmashauri wanafanya kazi zao kwa karibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wazo lake pia la kuwa na Maafisa Masoko tunalichukua, tutalifanyia tathmini na kuona kama tunaweza tukaongeza nguvu katika eneo hilo kuwa na maafisa biashara na pia kuwa na maafisa masoko. Kwasababu lengo la Serikali ni kuhakikisha kuna ufanisi mkubwa wa biashara na ustawi wa mapato ya ndani lakini pia ya wananchi katika masoko yetu.