Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 201 2021-05-06

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe hasa kwenye Idara za Afya, Elimu na Kilimo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Ikama ya mwaka 2020/2021, Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe inapaswa kuwa na watumishi 2,630. Hadi Machi 2021 Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ilikuwa na watumishi 2,294 hivyo ina upungufu wa watumishi 336 sawa na asilimia 12.8.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Ikama Idara ya Afya katika Halmashauri ya Wlaya ya Korogwe inapaswa kuwa na watumishi 392, na hadi Machi 2021 Idara ya Afya ilikuwa na watumishi 263 hivyo ina upungufu wa watumishi 129 sawa na asilimia 32.9. Idara za Elimu msingi na sekondari zinapaswa kuwa na watumishi 1891 lakini zina watumishi 1604 hivyo zina upungufu wa watumishi 287 sawa na asilimia 15.2. Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika inapaswa kuwa na watumishi 55 na ina watumishi 45 hivyo ina upungufu wa watumishi 10 sawa na asilimia 18.2.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeendelea kuajiri na kuwapnaga watumishi wa kada mbalimbali katika halmashauri nchini ambapo katika mwaka wa fedha 2020/21 watumishi 81 wapya waliajiriwa na kupangwa katika Halamshauri ya Wilaya ya Korogwe. Kati ya hao, watumishi 22 ni walimu wa sekondari, 35 shule za msingi, 6 watumishi wa kada za afya na Afisa Ugani 1 pamoja na 17 wa kada mbalimbali. Pamoja na jitihada hizo, katika Ikama ya mwaka 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya imetenga nafasi za ajira mpya 150 ambao watapangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe.