Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya ujenzi wa mradi mkubwa wa maji Handeni Trunk Main (HTM)?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Ndani ya Mkutano huu wa Tatu Serikali ilikuja hapa ikatoa majibu kwamba mradi huu wa HTM utaanza mwezi wa Aprili. Wananchi wamekuwa wakiniuliza mara kwa mara mwezi Aprili umepita na mradi haujaanza. Sasa kwenye majibu ya Serikali wanadai kwamba mradi utaanza kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha. Mwaka wa fedha unaisha mwezi mmoja mbele, naomba nijue ni lini hasa mradi huu utaanza kwa ajili ya wananchi wa Jimbo la Handeni? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, wananchi wa Jimbo la Handeni tuna dhiki kubwa ya maji na tumekuwa tukinywa maji kwenye mabwawa kwa miaka mingi lakini mabwawa haya pia yamebebwa na mvua katika misimu iliyopita. Bwawa la Kwimkambala pale Kwendyamba, Kumkole pale Mabanda pamoja na Bwana la Mandela pale Kwenjugo; yote haya yamebebwa na mvua.

Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa mabwawa haya ili wananchi angalau tuendelee kunywa maji tukisubiria Mradi huu wa HTM. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru lakini nimpongeze Naibu wangu kwa namna anavyojibu maswali. Kubwa nimpongeze sana kaka yangu Reuben amekuwa amefuatilia mradi huu mkubwa wa miji 28.

Mheshimiwa Spika, kesho nimewaalika Wabunge wote wanaohusiana na mradi huu wa miji 28 tuwape commitment na uelekeo mzima wa mradi huu. Kwa hiyo nimwombe sana kesho katika kikao ambacho tutakachokaa tutatoa commitment ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kubwa tunatambua kabisa kwa eneo la Handeni palitokea mafuriko yale mabawa yalikwenda na maji, Mheshimiwa Mbunge kwa udharura huo na sisi tuna pesa za dharura, naomba saa saba tukutane tuone namna ya kuweza kusaidia wananchi wake waweze kupata huduma ya maji. (Makofi)