Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 22 Water and Irrigation Wizara ya Maji 189 2021-05-04

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya ujenzi wa mradi mkubwa wa maji Handeni Trunk Main (HTM)?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Reuben Kwagilwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipata mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim, jumla ya Dola za Marekani milioni 500 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi katika miji 28 nchini ukiwemo Mradi wa Maji wa Kitaifa Handeni (Handeni Trunk Main) utakaohudumia vijiji 84 katika Wilaya ya Handeni pamoja na Miji Midogo ya Mkata, Komkonga, Kabuku, Michungwani,Segera pamoja na Mji wa Handeni.

Mheshimiwa Spika, taratibu za kupatikana kwa wakandarasi watakaotekeleza mradi huu zimekamilika na unatarajiwa kuanza wakati wowote katika mwaka wa fedha 2020/2021 na ujenzi wa mradi umepangwa kutekelezwa miezi 24.