Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na Sera na Mitaala shirikishi ili kuwa na msingi wa aina moja kuanzia elimu ya maandalizi, elimu msingi na sekondari kati ya Tanzania Bara na Zanzibar ili kuongeza ufaulu zaidi kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na nashukuru Serikali kwa hatua iliyofikia katika kurekebisha masuala ya sera na mitaala kwa pande mbilli za Muungano, hata hivyo na maswali mawili madogo sana ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, muda mrefu sana Baraza la Mitihani lilikuwa likiwasiliana moja kwa moja na vituo vya mitihani vya Zanzibar na mara nyingi Wizara ya Elimu bila kuwa na taarifa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuunda chombo maalumu cha kisheria ambacho kinatambulika ili kuweza kuunganisha Wizara ya Elimu ya Muungano na Wizara ya Elimu ya Zanzibar?

Mheshimiwa Spika swali langu la pili ni kuhusu elimu ya juu, katika Bunge la Kumi na Moja niliuliza na nikaambiwa linafanyiwa kazi kuhusu vyuo vikuu huria ambapo vilevile vyuo ambavyo vinatumika hapa na kutambulika na NACTE wale watu ambao wamefanya mitihani kupitia vyuo hivyo wanakubalika kufanya kazi Tanzania Bara na pia
wanatambulika kwamba wamesoma na vyeti vyao vinatambulika lakini kwa Zanzibar havitambuliki. Je, suala hili limefikia wapi? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Giga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) ni Taasisi ya Muungano ambayo inaendesha mitihani hapa nchini. Baraza la Mitihani lina muundo wa namna ya kuendesha shughuli zake; tunakuwa na Kamati za Mitihani ngazi ya Taifa, Mikoa na Wilaya. Kamati hizi ndizo ambazo zinafanya ule mtiririko wa mawasiliano na mahusiano katika uendeshaji wa shughuli za Baraza la Mitihani. Kwa hiyo, kimsingi vyombo vipo, kwa kutumia Kamati hizi; ndizo ambazo zinaratibu pamoja na kuendesha mitihani kote nchini ikiwemo Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Mheshimiwa Spika, Baraza la Mitihani lina watumishi kule Zanzibar na vilevile tuna ofisi pale Zanzibar katika jengo lile la Shirika la Bima Zanzibar. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba Baraza la Mitihani limejipanga vizuri na namna bora ya mawasiliano pamoja na co-ordination ni kama hivyo nilivyoeleza.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili, kwamba kuna vyuo ambavyo havitambuliwi na NACTE; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vyuo vyote vya elimu ya kati ambavyo vinahusika na masuala haya ya NACTE vimesajiliwa na NACTE na orodha ya vyuo hivyo ipo kwenye website.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namqomba tu Mheshimiwa Mbunge labda tuweze kukaa na kuangalia kuna changamoto zipi kule Zanzibar ambapo labda kuna vyuo ambavyo havijapata usajili ili tuweze kujua kitu gani cha kufanya. Nakushukuru sana.