Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Serikali inafahamu madhara yatokanayo na madini ya zebaki?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ninalo ninakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ningependa kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa, Serikali inayafahamu kwa kuyataja kabisa madhara yanayotokana na kemikali ya zebaki lakini pia kwa kuwa, kutumia njia hii kuchenjulia dhahabu tunapata asilimia kidogo tu kama ambazo ametaja asilimia 30, ni kwanini sasa Serikali isitumie cyanide kuchenjulia madini hayo ya zebaki na kuachana na kemikali hatari ya zebaki? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili, kibali cha ku-import kemikali ya zebaki nchini kinatolewa na Mkemia Mkuu wa Serikali. Wataalam kutoka Wizarani wanatuambia kwamba Mkemia Mkuu wa Serikali hakupokea maombi ya ku-import zebaki nchini. Cha ajabu ni kwamba, kemikali hiyo ipo ya kutosha tu huko mtaani, sasa ni nini kauli ya Serikali juu ya njia hizi za panya zinazoingiza kemikali hii kiholela? Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, cyanide pamoja na baadhi ya acids ndio njia sahihi ambayo inafaa kwa ajili ya uchenjuaji dhahabu kwa sasa na ndio teknolojia ambayo aaah! Kama Mheshimiwa Mchafu atakumbuka kwamba, ndio teknolojia mpya ambayo imetumika na ndio imeleta hasa manufaa kwa wachimbaji wadogo. Sema, kwa kutumia cyanide pamoja na vat leaching inakuwa inahitaji kidogo mtaji uwe mkubwa ili mchimbaji mdogo aweze kuitumia. Sasa kitendo cha kuhitaji mtaji mkubwa kidogo ndicho kinachofanya wengine bado wanaendelea kutumia mercury.

Mheshimiwa Spika, lakini ni kweli kwamba, wengi wameshaanza kuhama na ndio msisitizo wa Wizara tunawasisitiza watoke kule kwasababu ya madhara ambayo yanaonekana. Nikweli kwamba, kwa kutumia vat leaching ambayo inatumia cyanide ni kwamba, hata recovery inakuwa ni kubwa na kwa hiyo tumuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kama Wizara tutaendelea kufanya jitihada za kutoa elimu. Kwanza, wachimbaji wadogo wajue madhara makubwa yanayotokana na kutumia mercury, lakini pia ikiwezekana hata kama ni kujiunga kwa vikundi waende katika teknolojia ambayo inafanya recovery kubwa lakini pia haina madhara makubwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kweli kwamba mercury inapatikana kwa wachimbaji wadogo wakiitumia na kwasababu, kibali kilipaswa kutoka kwa Mkemia Mkuu kama ambavyo anatoa kuhusu kemikali zingine zozote zile. Lakini Mheshimiwa Mbunge anathibitisha kwamba sio kweli kwamba yeye ametoa vibali. Tulichukue kama Serikali kwasababu tunatamani kulinda mazingira yetu, tunatamani kuwalinda wachimbaji wetu ili tuingie katika mnyororo na ikiwezekana badala ya kutoa elimu kwenye matumizi, basi twende pia kuangalia hata source ya mahali ambapo zebaki inaingilia. Nadhani kwa jinsi hiyo tutaweza kuwasaidia maana yake ni kwamba tuanze udhibiti tangu kwenye source kuliko kule kwenye matumizi yenyewe kwa kujali afya na mazingira yetu. Ahsante (Makofi)

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Serikali inafahamu madhara yatokanayo na madini ya zebaki?

Supplementary Question 2

MHE. KABULA E. SHITOBELA: Mheshimiwa Spika, ahsante ukizingatia sisi ndio mama zako au bibi zako lazima uturuhusu ahsante sana. Kutokana na shughuli za uchimbaji madini Mkoani Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla, tatizo na ongezeko kubwa la kansa kwa Mkoa mzima wa Mwanza kumekuwa na tatizo kubwa la kansa na tunaamini kabisa hii zebaki ndio inayosababisha ongezeko hili la kansa. Je. Serikali ina mpango gani sasa wa kudhibiti kabisa uingiaji wa kemikali hizi, ili kunusuru wananchi wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla? (Makofi)

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Kabula kwa swali lake ambapo ameulizia kuhusiana na udhibiti.

Mheshimiwa Spika, kama alivyoeleza Mheshimiwa Naibu Waziri, hatua ya kwanza tuliyochukua mahali ambako dhahabu inachenjuliwa, inaitwa mialo, mwanzo mialo ilikuwa holela, kila mahali mtu anajenga; sasa tumeamua kuidhibiti ile mialo yote iwekwe kwenye eneo maalum na jumla ya mialo 5,025 imesajiliwa kote nchini.

Mheshimiwa Spika, pili, Chama cha Wachimbaji Wadogo kinaitwa FEMATA pamoja na Mkemia Mkuu wa Serikali wanatengeneza umbrella moja ya namna ya kuagiza zebaki hapa nchini na Mkemia Mkuu wa Serikali ameshatoa hiyo go-ahead lakini changamoto tuliyonayo ni ndogo ndogo tu ya uratibu. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ndani ya miezi hii miwili uagizaji wa zebaki tutakuwa tumeudhibiti na tutakuwa na source inayoeleka.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)