Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza naomba niishukuru Serikali kwa kuwa mradi huu wa Likuyusekamaganga ambao ulitumia muda mrefu umeanza kuonyesha dalili na sasa vituo vitano vinatoa maji kati ya vituo hamsini na tatu vilivyopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili (a) na (b);

(a) Kwa kuwa mradi wa Njoomlole, Ligunga, Lusewa na Kanjele mabomba yametandazwa ila tunapewa sababu ya kutokuwa na viunganishi katika mradi huo. Je, Serikali viunganishi hivi vinatoka wapi kwa nini wasituletee mara moja ili watu wapate maji? (Makofi)

(b) Swali la pili, kwa upande wa Mji wa Namtumbo, vitongoji vyake na maeneo la Rwinga, Minazini, Lusenti, Libango, Suluti na Luegu wanapata maji mara moja kwa wiki mgao wake ni mkubwa sana na watu wanalalamika sana.

Je, Serikali inaweza ikafanya uboreshaji wa huu wa haraka ili wananchi wapate maji inavyotakiwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, mabomba ni kweli yametandazwa na hivi viunganishi tayari na vyenyewe vimeshafika hapa nchini. Nipende kumuagiza Meneja wa Mkoa wa RUASA – Ruvuma kuhakikisha mradi huu anakwenda kuukamilisha mara moja na maji sasa yaweze kuwafikia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lako la pili, umeongelea kuhusiana na ule mgao mkali wa mara moja kwa wiki, tayari sisi kama wizara tumeendelea kujipanga kuhakikisha mgao wa maji maeneo yote yanakwenda kushughulikiwa na tunapunguza hayo maumivu ya mgao wa maji. Na hili pia ninamuagiza RM – Ruvuma kuhakikisha anaendelea kuona namna bora ya kufanya kupitia vyanzo tulivyonavyo kuhakikisha mgao huu unapungua kutoka mara moja kwa wiki angalau mara nne kwa wiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vile vile nipende kuagiza mameneja wa Mikoa wote hata pale Mwanza kwenye Jimbo la Ilemela maeneo ya Ilalila, Kahama, Nyamadoka, nahitaji kuona kwamba kila mmoja anawajibika vema. Kwa hiyo, mameneja wote wa Mikoa waweze kuhakikisha wanawajibika na maji yanaweza kuwafikia wananchi. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona, kwa kuwa tatizo la maji lililopo katika Jimbo la Namtumbo linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati katika Kata ya Riroda, Duru, Hoshan, Gidas, Hewasi.

Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya maji yaliyopo katika maeneo hayo ili kumtua mama ndoo kichwani? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali lengo jema kutoka Wizara ya Maji ni kuona kwamba miradi yote ambayo inatekelezwa inakamilika kwa wakati. Kwa hiyo, hii miradi ambayo ipo Babati inaendelea na utekelezaji itakamilika kulingana na muda wake wa utekelezaji namna ambavyo usanifu ulionyesha.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwenye hili suala la maji, ninashukuru sana kwamba matatizo haya yanayotokea kwenye Jimbo la Namtumbo yanafanana sawa kabisa na matatizo yaliyopo Jimbo la Ndanda hasa kwenye Kata za Mlingula, Msikisi, Namajani pamoja na vijiji vyake. Ninataka kufahamu sasa mpango mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kabla ya kiangazi kikuu tunapata maji ya kutosha na uhakikisha kwenye maeneo haya. Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tatizo la maji linapungua. Na ndiyo maana Wizara ya Maji iliweza kuunda chombo hiki cha kushughulikia maji vijijini pamoja na usafi wa mazingira kwa maana ya RUASA. Hivyo maeneo yote ambayo kwa sasa hivi yamekuwa yakipitia changamoto ya maji tunaendelea kuyashughulikia kwa karibu kabisa kwa nia ya dhati kuona kwamba tatizo la maji tunakwenda kulipunguza kama si kulimaliza.

Mheshimiwa Naibu Spika, basi na maeneo ya Ndanda kama tulivyoongea Mheshimiwa Mbunge nimekuahidi kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha tutakuja angalau tuanze na kisima kimoja, viwili. Lakini mpango wa muda mrefu ni utaanza mwaka ujao wa fedha.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulizwe swali la nyongeza kwenye Wizara hii ya Maji.

Kwa kuwa Wilaya ya Longido ni moja ya wilaya kame sana nchini na kwa kuwa tuna baadhi ya milima ambayo inavyanzo vya chemchem kwenye misitu ya Serikali kama mlima Gilay, Mlima Kitumbeine, Mlima Longido na chemchem iliyopo matali A na chemchem zinazotoka upande wa West Kilimanjaro Kata za Ormololi na Kamwanga na kuna mabonde ambayo yangeweza kuchimba mabwawa pamoja na visima kirefu... (Makofi)

NAIBU SPIKA: Swali Mheshimiwa.

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Je, Serikali ina mpango kusaidia kumaliza kero ya maji kwa wananchi wa Jimbo la Longido.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Steven Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kuona kwamba maeneo yote ambayo yana matatizo ya maji tunakwenda kuyashughulikia. Mheshimiwa Dkt. Steven tumekuwa tukiwasiliana kwa karibu na nampongeza sana kwa ufuatiliaji wake wa karibu wa suala hili. Nachoweza kumhakikishia kama tulivyozungumza, Kijiji cha Opkeli, Kata ya Mundarata; Kijiji cha Ogira, Kitongoji cha Ingokin, maeneo haya yote tunakwenda kuyashughulikia. Lengo ni kuona maeneo yale yote maji yanakwenda kutoka bombani iwe kwa chanzo cha maji cha kisima ama chanzo kingine cha maji.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 5

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mloo wenye wakazi zaidi ya 70,000 unakabiliwa na changamoto kubwa sana ya maji. Naomba kufahamu nini mpango wa Serikali katika kuwatua ndoo wanawake wa Mji Mdogo wa Mloo? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeendelea kutoa maelekezo na kutekeleza miradi maeneo ya Mloo mpaka Tunduma. Kote huko tunaendelea kuhakikisha maji yanakwenda kupatikana. Katika maeneo ambayo nimefanya ziara yangu ya awali kabisa ni Mloo pamoja na Tunduma. Tayari tumemsimamisha yule mtumishi ambaye hakuwa tayari kuendana na kasi ya sasa na tukamweka pale Meneja wa Mkoa wa RUWASA kwa sababu ni mtendaji mzuri. Pia tayari mkeka tumeshauandaa tunaenda kuongeza timu maeneo yale ya Mloo na Tunduma ili kuhakikisha maji yanakwenda kutoka.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 6

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Kwa kuwa, tatizo la maji katika Jimbo la Serengeti ni sawa kabisa na tatizo la maji kule Namtumbo. Naipongeza sana Wizara, rafiki yangu Mheshimiwa Jumaa amejitahidi sana kuhakikisha mradi wetu wa maji hasa ule wa chujio unakamilika hata hivyo mpaka sasa hivi mradi ule bado haujakamilika, lakini pia kupeleka maji katika vijiji vya Jirani. Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi yote hii miwili?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri wangu kwa namna bora na nzuri ya kujibu maswali. Kweli nimeamini mtoto wa samaki hafundishwi kuogelea, hongera sana Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kubwa ambalo nataka niliseme ni kwamba Wizara ya Maji tumepokea miradi 177 ambayo ni kichefuchefu na ilikuwa ikichafua Wizara. Mkakati wa Wizara baada ya kuanzisha Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA), tukasema miradi hii yote kichefuchefu ikiwemo mradi wa Mugumu ambao ulikuwa ukichafua, sasa hivi tunaukwamua. Katika wiki hii tunatoa fedha zaidi ya milioni 300 kuhakikisha tunakamilisha mradi ule na wananchi wa Mugumu waweze kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)