Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 160 2021-04-29

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-

Jimbo la Namtumbo lina tatizo la maji karibu maeneo yote ya Vijijini pamoja na Makao Makuu ya Wilaya: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika bajeti ya mwaka 2020/2021?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya Maji vijijini Wilayani Namtumbo ni asilimia 69. Katika kutatua tatizo la maji Jimbo la Namtumbo, Serikali Katika mwaka wa fedha 2020/2021 kupitia RUWASA imekamilisha miradi miwili, ambayo ni mradi wa maji Mkongogulioni - Nahimba na mradi wa maji Mtakuja. Miradi hiyo itahudumia jumla ya wananchi 9,683 katika vijiji vya Mkongogulioni, Nahimba na Mtakuja. Utekelezaji wa miradi ya maji ya Likuyusekamaganga, Njoomlole, Ligunga, Lusewa na Kanjele unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2021 na miradi ya Litola – Kumbura, Luhimbalilo – Naikesi, inatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Mji wa Namtumbo Serikali inaendelea na mipango ya muda mfupi na muda mrefu. Kwa muda mfupi utekelezaji wa mradi wa uboreshaji, ambapo bomba kuu na mabomba kwa ajili ya usambazaji yamelazwa umbali wa kilometa 31.92 na umegharimu Shilingi milioni 653.2. Pia, kazi ya kuunga wateja 1500 katika urefu wa bomba kilometa 24 inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mpango wa muda mrefu, Serikali imepanga kutekeleza mradi mkubwa kwa ajili ya maji kutoka vyanzo vya maji vya Likiwigi na Libula vyenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya Lita Milioni Nne kwa siku. Usanifu wa mradi umekamilika na ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2021/2022.