Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Daraja kwenye Mto Malagarasi ili kuunganisha Kata ya Ilagara na Kata ya Sunuka katika Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa usanifu ulikamilika na kuwa usanifu unaofanyika ni uhuishaji wa usanifu wa awali. Je, Serikali haioni haja kutenga fedha mwaka ujao wa fedha ili kujenga daraja hilo 2021/2022 ili kunusuru maisha ya wanawake na watoto wanaopoteza maisha kwasababu ya kutokuwa na kivuko hicho?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Kwa kuwa, kivuko kinaanca kazi saa 01:00 asubuhi na kuishia saa 01:00 jioni. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza saa ili kivuko hicho kifikie saa 06:00 usiku kuweza kuwanusuru wananchi wanaopoteza maisha kutokana na saa hizo kuwa fupi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye jibu langu la msingi nimeeleza kwamba, tumetenga, kama bajeti itapitishwa kama ilivyoombwa, tumetenga milioni 400 kukamilisha usanifu wa kina.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nimueleze Mheshimiwa Mbunge kwamba, daraja hili ni kati ya madaraja makubwa yatakayojengwa Tanzania, Mto Malagarasi ni kati ya mito mikubwa katika Tanzania hivyo, tutakapokamilisha usanifu wa kina ndio ujenzi utaanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kivuko kinafanya kazi kuanzia saa 01.00 hadi saa 01.00 jioni.

Mheshimiwa Naibu Spika, naungananae, na kwasababu ya changamoto ya Mto Malagarasi ambao ni mto mkubwa una zaidi ya kilometa 300 na unapita kwenye misitu mikubwa ambayo inabeba magogo na miti, lakini pia kuna wakati unafurika na mpaka zile sehemu zake za ku-park vile viuvuko huwa hazipo ndio maana Serikali imeona isifanye kazi usiku kwasababu, inaweza ikapeleka kivuko ziwani na hata kukipindua hicho kivuko kwa sababu ya hayo magogo na miti.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa anafahamu kwamba tumeweka utaratibu pale ambapo kuna dharura, watu hao wapo na wamekuwa wanafanya kazi. Hata hivyo, ili kuondokana na changamoto hiyo kabisa ndiyo maana Serikali sasa imekuja na mpango wa kujenga daraja, ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Daraja kwenye Mto Malagarasi ili kuunganisha Kata ya Ilagara na Kata ya Sunuka katika Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona kwa ajili ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kivuko hiki cha Mto Malagarasi ni muhimu kama ilivyo barabara ya kutoka Kilosa – Magomeni – Masanze -Zombo – Ulaya - Muhenda – Mikumi. Pia barabara hii ilikuwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi mwaka 2015-2020 na ipo kwenye Ilani 2020-2025 na ipo kwenye bajeti…

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, je ni lini ujenzi wa barabara hii unaenda kuanza? Nashukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja imeainishwa kwenye Ilani lakini pia ipo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dennis Londo kwamba kuanzia bajeti hii tutakayoianza barabara hii itaanza kufanyiwa kazi kwenye mipango yetu kwani viongozi wengi wameahidi barabara hiyo ijengwe. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi yeye na wananchi wa Mikumi kwamba barabara hii ipo kwenye mpango na itatekelezwa katika kipindi hiki cha miaka mitano.