Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 18 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 155 2021-04-28

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja kwenye Mto Malagarasi ili kuunganisha Kata ya Ilagara na Kata ya Sunuka katika Wilaya ya Uvinza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephine, Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Daraja la Malagarasi (Lower Malagarasi Bridge) linaunganisha Kata ya Ilagala na Kata ya Sunuka katika Wilaya ya Uvinza kupitia Barabara ya Simbo – Ilagala hadi Kalya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa daraja hili katika bajeti ya mwaka huu wa 2020/2021, Wizara yangu imetenga shilingi milioni 345 kwa ajili ya kufanya kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa Daraja hili la Malagarasi. Aidha, katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2021/2022 daraja hili limetengewa shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuendelea na kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina. Kwa sasa taratibu za ununuzi wa Mhandisi Mshauri wa kufanya kazi hiyo zinaendelea. Baada ya kazi hiyo kukamilika, ujenzi wa daraja hili utaanza kadiri ya upatikanaji wa fedha utakavyokuwa. Asante.