Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italiangalia zao la asali na kulitafutia soko la uhakika ndani na nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na jitihada nzuri za Wizara inavyofanya kuzitangaza zao la asali nchini, lakini bado hatujafanya vizuri kwa masoko ya nje ambayo inapelekea wafanyabiashara wengi wa nchini wanashindwa kufanya vizuri kwa masoko ya nje hususan ni Mkoa wa Tabora na tukiangalia kinamama wengi wa Mkoa wa Tabora wamejikita kwenye uvunaji wa asali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Wizara inakuja na mkakati upi kuhakikisha soko la nje la zao la asali linafanya vizuri kama ambavyo zao la asali linafanya vizuri ndani ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, pamoja na jitihada nzuri zinazofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuhakikisha zao la asali linaendelea kuwa na thamani, mpaka kupata wafadhili kutoka Umoja wa Ulaya.

Je, Wizara imeweka mikakati ipi na mipango madhubuti ya kutenga pesa kwa ajili ya kuhakikisha mradi huu walioweka kusaidiwa na Umoja wa Ulaya unaweza kuendelea hata kama mradi ule, hata kama wafadhali watachelewesha pesa au hawatoleta pesa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline, Mbunge wa Viti Maalum Tabora kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora Mheshimiwa Jacqueline kwa kuona umuhimu wa zao hili la asali. Ni kweli Tanzania tunafaidika kwa asilimia kubwa kwa soko hili la asali kuuza ndani na nje ya nchi. Mkakakati wa Wizara na Serikali kwa ujumla ni kuhakikisha kwamba asali yetu inakuwa na ubora zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge ni kwamba kwa sasa hivi wizara inashikirikiana na Umoja wa Ulaya ikiwemo Ujerumani kupeleka sampuli za kemikali za asali ambazo huwa zinachakatwa na kuangalia ubora wa asali ya Tanzania. Na kwa asilimia 90 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 tulipeleka asali yetu ya Tanzania na ikaonekana kwa asilimia 90 ni nzuri na inafaa kuuzwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba Tanzania sasa itaanza kupeleka asali kwenye nchi za Ulaya na Marekani kwa kuwa tumekidhi vigezo vya viwango vya ubora wa asali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwenye mikakati ya kutenga fedha nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sasa tuna mkakati wa kuanzisha viwanda vitano. Viwanda vitatu tayari vimeshajengwa na viwili tunakarabati. Lakini pia hii ni mwanzo wa kuhakikisha kwamba tayari tuna vyanzo vyetu sisi wenyewe bila kutegemea misaada mingine ambavyo vitaweza kukusanya asali yote nchini na itachakatwa kwenye viwanda hivi na kuhakikisha soko la ubora wa asali linapatikana na tunaweza kuuza nje na ndani ya nchi. Ahsante. (Makofi)

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italiangalia zao la asali na kulitafutia soko la uhakika ndani na nje ya nchi?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Makao Makuu ya TANAPA Kanda ya Magharibi yako Bunda; na kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Bunda ilitoa eneo kwa ajili ya kujenga ofisi zao za Kanda ya Magharibi. Je, ni lini TANAPA wataanza kujenga ofisi hizo? (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nimshukuru Mheshimiwa Robert Maboto kwa swali lake hilo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, TANAPA ina kanda nyingi nchi nzima na kila kanda inahitaji fedha ili tuweze kujenga miundombinu husika. Katika bajeti ambayo tutaileta mwaka huu tumeomba fedha kutoka Hazina ambazo ni mahsusi kwa ajili ya kujenga na kuboresha miundombinu ikiwemo Ofisi ya Kanda ya TANAPA pale Bunda.