Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji wa Kintinku – Lisilile ili wananchi wa vijiji 11 vya Kata za Chikuyu, Makutupora, Maweni na Kintinku waanze kupata maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, natumia nafasi hii kumshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa huu mradi umechukua muda mrefu sana, zaidi ya miaka kumi, kukamilika, na kwa kuwa Waziri ameahidi kwamba ndani ya huu mwaka mmoja huu mradi unakuja kukamilika; ninapenda kujua sasa Wizara inakuja na mikakati gani ndani ya huu mwaka mmoja kuhakikisha maji yanafika katika vijiji 11.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa huu mradi vilevile unanufaisha kata tatu ambazo zina miradi mikubwa ya kimkakati ukiwepo mradi wa ujenzi wa reli lakini vilevile na kituo cha afya. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa haraka kupeleka maji katika Kata ya Kintinku na Maweni?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Naibu Waziri wangu kwa kazi kubwa na nzuri namna anavyojibu maswali yake, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilifanya ziara katika Mradi wa Kintiku-Lusilile, ni mradi ambao umechukua muda mrefu sana na mkandarasi alikuwa akidai kiasi cha pesa. Tumeweza kumlipa kiasi cha shilingi milioni 500, lakini pia tumepokea fedha shilingi bilioni 25, kwa ajili ya kuwalipa wakandarasi. Nataka nimhakikishie mmoja wa wakandarasi ambao watalipwa fedha ni Mradi huu wa Kintiku-Lusilile. Kwa hiyo maelekezo ya Wizara na wakandarasi wote watakaopata fedha ni kuhakikisha wanakamilisha miradi kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ruhusa yako nataka niliambie Bunge lako Tukufu jana Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo mahususi katika Wizara yetu ya Maji, na sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji tumeyapokea na tutayafanyia kazi kikamilifu. Lakini naomba nitume salamu kwa wahandisi wa maji pamoja na wakandarasi; wakae mguu sawa, na sisi tutafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana. (Makofi)