Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 135 2021-04-23

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji wa Kintinku – Lisilile ili wananchi wa vijiji 11 vya Kata za Chikuyu, Makutupora, Maweni na Kintinku waanze kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Kintinku- Lusilile ni mradi mkubwa ambao unatekelezwa kwa awamu nne na hadi mwezi Machi, 2021 utekelezaji wa awamu ya kwanza umefikia asilimia 90 kwa gharama ya shilingi bilioni 2.085. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ufungaji wa mitambo ya kusukuma maji, ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji, tanki la kukusanya maji la lita 300,000 na ujenzi wa tanki la kuhifadhi na kusambaza maji la lita milioni mbili na ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilometa 1.2. Aidha, vijiji vitatu vya Chikuyu, Mwiboo na Mbwasa vinatarajiwa kuanza kupata huduma ya maji mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia RUWASA imepanga kukamilisha usambazaji wa maji katika vijiji vyote 11 katika mwaka wa fedha 2021/22 na utahudumia wakazi zaidi ya 55,000.