Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka vitendea kazi Kituo cha Afya Kata ya Mtii, Jimbo la Same Mashariki baada ya kukamilika kwa vyumba 12 vya Jengo la OPD?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwashukuru sana wananchi wa Kata ya Mtikwa kunipa kura nyingi sana bila shuruti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kuuliza swali la nyongeza kwa kuwa jumatatu ya pasaka mimi na Naibu Waziri wa Afya tulikwenda kuiona zahanati hii ya Kata ya Mtii na kwa kuwa wananchi wale wamefanya jitihada, niliyeanza kujenga ile zahanati ni mimi na wananchi, sasa wananchi walichomlilia Naibu Waziri wa Afya, wanaomba wajengewe nyumba ya Mganga.

Je, Serikali hamuoni kwamba wananchi wangu wamejitahidi sana kujenga zahanati ile wao wenyewe na Mbunge wao na Mbunge alipokuja aliweka kitu kidogo mkatusaidia kujenga nyumba ya mganga wa zahanati ile? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeza sana Mheshimiwa Mbunge Anne Kilango Malecela na wananchi wa Jimbo la Same Mashariki kwa kazi kubwa walioifanya kuanzaujenzi wa Zahanati ya Mtii, lakini nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge amekuwa karibu sana na wananchi, amefanya ziara pale na Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya na wameona kazi nzuri inayoendelea na wananchi wanatambua mchango mkubwa wa Serikali ambao unaendelea kutolewa katika ujenzi wa zahanati ile.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyojibu kwenye swali la msingi tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya Zahanati ya Mtii, lakini pamoja na kuweka bajeti kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mganga katika zahanati ile. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka vitendea kazi Kituo cha Afya Kata ya Mtii, Jimbo la Same Mashariki baada ya kukamilika kwa vyumba 12 vya Jengo la OPD?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Njombe Mjini na sisi tuna Kituo cha Afya ambacho kina uhitaji wa wodi ya kibaba na wazazi na huduma ya upasuaji na Serikali ilishaonesha nia ya kutusaidia.

Swali, je, ni lini sasa shughuli ya ujenzi na ukarabati wa kituo cha afya cha muda mrefu sana Njombe Mjini utaanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba katika Jimbo la Njombe Mjini kuna Kituo cha Afya cha Mji Mwema na cha siku nyingi ambacho kina uhitaji mkubwa wa miundombinu ya wodi ya akina baba akina mama lakini na wodi ya watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti ya mwaka huu wa fedha tumetenga fedha kwa ajili ya kwenda pia kuongeza miundombinu katika Vituo vya Afya na nimuhakikishie kwamba Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Jimbo la Njombe Mjini nacho kitapewa kipaumbele.