Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 131 2021-04-23

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka vitendea kazi Kituo cha Afya Kata ya Mtii, Jimbo la Same Mashariki baada ya kukamilika kwa vyumba 12 vya Jengo la OPD?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuweka kumbukumbu sahihi kwanza naomba nianze kwa ufafanuzi kwamba jengo linalojengwa eneo la Mtii ni zahanati na si kituo cha afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zahanati ya mpya inayojengwa kwa nguvu za wananchi, fedha za Mfuko wa Jimbo, wadau wa maendeelo pamoja na fedha za Halmashauri. Majengo yanayojengwa ni pamoja na Jengo la Wagonjwa wa Nje na Jengo la Huduma ya Kliniki ya Afya ya Mama na Mtoto ambayo tayari yamekamilika na ujenzi wa Jengo la Huduma za Uzazi unaendelea. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Same imepokea fedha shilingi milioni 150 iliyotengwa kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 ambapo Zahanati ya Mtii imepokea shilingi milioni 50 itakayotumika kukamilisha Jengo la Wazazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Zahanati ya Mtii itakapokamilika itapatiwa usajili na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kuwekewa utaratibu wa kupatiwa vitendea kazi.

Aidha, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele cha ununuzi wa vifaa tiba katika Hospitali za Halmashauri na Vituo vya Afya vilivyojengwa na kukarabatiwa na kote nchini, vikiwemo Vituo vya Afya vya Ndungu, Shengena na Kisiwani ambavyo vimepokea shilingi milioni 400 kila kimoja na Zahanati ya Kasapo iliyopokea shilingi milioni 154 vilivyoko kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Same ambavyo tayari vimepokea fedha hizo na shughuli za ujenzi zinaendelea ujenzi na ukarabati wa vituo hivyo umekamilika na huduma sasa zinatolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Halmashauri ya Wilaya ya Same iweke kipaumbele kwa kutenga bajeti kwa kupitia mapato yake ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba vya zahanati mpya ya Mtii pindi itakapokamailika na kupatiwa usajili.