Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Mifuko ya Kuendeleza Utalii na Wanyamapori na kufikia lengo la watalii milioni tano ifikapo 2025?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kama unavyokumbuka kwamba mifuko hii imeweza kuchangia maendeleo makubwa katika masuala ya uhifadhi, hususan kupunguza wimbi la ujangili nchini pamoja na kuongeza wigo wa masuala mazima ya miradi ya wanajamii, halikadhalika kuingiza vivutio ambavyo vimetupelekea kufikia lengo la watalii 1,300,000: Je, kutokana na mabadiliko ya sheria hii, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba mabadiliko haya hayaendi kudumaza maendeleo ambayo yamefikiwa katika matumizi ya mifuko inayoathirika kutokana na sheria hii?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kama tunavyofahamu, mwezi wa Pili mwaka huu Mheshimiwa Waziri Mkuu alifungua maonyesho ya mifuko pale Arusha na alitoa wito wa kwamba mifuko hii iweze kuendelezwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Je, tuna mpango gani mbadala wa kuisaidia mifuko hii ili pamoja na mabadiliko haya ya sheria ambayo yamefanyika kuhakikisha kwamba yanakwenda kusaidia mafanikio ambayo yamepatikana hasa tukilinganisha kwamba hivi sasa wenzetu wa CMA wameanza kulalamika kutokana na matatizo ya...?

SPIKA: Ahsante sana. Umeshaeleweka Mheshimiwa.

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. kwanza nashukuru kwa swali la Mheshimiwa Soud, lakini nimtoe wasiwasi kwamba Serikali iliona suala hili baada ya mifuko hii fedha zake zilizokuwa zinakusanywa kupelekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina, Serikali ilianza kutekeleza majukumu yake yaliyokuwa yanatekelezwa kwenye mfuko huu kupitia bajeti ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi kwamba shughuli sasa ambazo zilikuwa zinatekelezwa na mfuko huu ikiwemo uhifadhi, kudhibiti ujangili na shughuli nyingine za kuendeleza utalii, kukuza na kutangaza utalii, Shughuli zote hizi sasa zinatekelezwa na bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 shughuli zote zilizokuwa zinatekelezwa kwenye mifuko hii, sasa zimeingizwa kwenye bajeti kuu ya Serikali. Naomba kuwasilisha.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Mifuko ya Kuendeleza Utalii na Wanyamapori na kufikia lengo la watalii milioni tano ifikapo 2025?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na kumwalika Naibu Waziri aje kutembelea msitu wa hifadhi wa Rondo, maeneo ya Tarafa ya Rondo, Rutamba, Milola na Kiwawa yamekuwa yakiathiriwa sana na Wanyamapori hasa tembo; na kwa kuwa idadi ya askari wanaohusika na ulinzi wa eneo hili ni kidogo.

Je, Serikali iko tayari kutoa mafunzo na kuwawezesha vijana wa maeneo haya washirikiane na wale askari katika kusaidia kulinda mali na Maisha ya wananchi wa eneo hili?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa
Spika, ahsante. Ni kweli kumekuwa na matukio mbalimbali ya uvamizi wa tembo. Hii tukumbuke tu kwamba tunaishi maeneo mengi ambayo kihistoria ilikuwa ni mapito ya Wanyamapori wakiwemo tembo. Wizara kwa mara nyingi imekuwa ikipata hizi taarifa na kutoa ushirikiano kwa wananchi ikiwemo kupeleka maaskari kuwaondoa hao tembo.

Mheshimiwa Spika, Serikali iko tayari kushirikiana na vijana wakiwemo kwenye maeneo husika hasa kuanzisha WMA ambazo huwa zinashirikiana na Wizara katika kuhakikisha kwamba zinatunza maeneo husika lakini pia tunashirikiana kudhibiti hawa Wanyama wakali. Hivyo niko tayari kuongozana na Mheshiniwa Nape Nauye kwenye Jimbo lake kuhakikisha kwamba suala hili tunali-solve kwa Pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Mifuko ya Kuendeleza Utalii na Wanyamapori na kufikia lengo la watalii milioni tano ifikapo 2025?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Miaka 20 iliyopita ndani ya Jimbo la Momba Ivuna, kuna kimondo kidogo kilidondoka (Ivuna Meteorite) na kikachukuliwa na watu wa NASA. Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia kimondo hiki kwa ajili ya kukirudisha na kuendelea kuongeza idadi ya watalii nchini? (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nampongeza kwanza Mheshimiwa Condester kwa kazi nzuri anayowafanyia wananchi wa Momba na ndiyo maana walikuchagua kwa kura nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imeshaanza kufanya mawasiliano na Balozi wetu aliyeko nchini Marekani kuanza kufuatilia jambo hili. Tutakapopata majibu, tutamjulisha Mheshimiwa Condester na Bunge lako Tukufu. Ahsante.