Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Mto Ruvuma kwa Wananchi wa Mtwara ili kuondoa shida ya maji iliyodumu kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali langu la kwanza: Serikali ilianza mpango wa kulipa fidia kwa wananchi wa Mtwara Vijijini waliopitiwa na bomba la maji kutoka Mto Ruvuma mwaka 2015. Nataka kujua, mradi huu umekwama wapi ikiwa tayari wananchi walishaanza kufanyiwa uthamini ili mradi huo uanze? (Makofi)

Swali la pili: Fedha zilizotengwa ili kutekeleza mradi wa maji wa Mto Ruvuma ambapo wananchi walishaanza kupewa utaratibu wa malipo ya fidia mwaka 2015 zimeenda wapi? Serikali inawaambia nini wananchi wa Mtwara Vijijini kuhusu mradi huo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli fidia hii ilianza kutekelezwa mwaka 2015. Mradi huu wa Mto Ruvuma ni ile miradi mikubwa ambayo mkakati wake lazima uwe madhubuti ili mradi usiishie njiani. Hivyo fidia namna ambavyo baadhi wameshalipwa, wale ambao bado hawajalipwa nao wanakuja kukamilishiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, kufikia mwaka ujao wa fedha 2021/2022 tumeweka mikakati ya kuona kwamba, tunakuja sasa kukamilisha miradi ya maziwa makuu ikiwepo mradi wa Mto Ruvuma pamoja na miradi mingine. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Mto Ruvuma kwa Wananchi wa Mtwara ili kuondoa shida ya maji iliyodumu kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Wilaya ya Kilwa kuna changamoto inayofanana na Wilaya ya Mtwara katika huduma hii ya maji:-

Je, Serikali ni lini itatekeleza mradi wa maji kutoka Mto Rufiji ili kuwaondolea changamoto ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Kilwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Serikali ina mipango mikakati ya kuona kwamba Mto Rufiji iwe ni sehemu ya miradi mikubwa ya kutoka maziwa makuu na mito, kuona kwamba maji yale sasa yanakwenda kunufaisha wananchi. Hivyo, kwa watu wa Kilwa pia tunaendelea kuwasihi waendelee kutuvumilia kidogo, huenda mwaka 2021/2022 kadiri tutakavyokuwa tunapata fedha, watu wa Kilwa pia watapata maji kupitia Mto Rufiji. (Makofi)