Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 107 2021-04-20

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Mto Ruvuma kwa Wananchi wa Mtwara ili kuondoa shida ya maji iliyodumu kwa muda mrefu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati ambapo Serikali inatarajia kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha 2021/2022 kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika kuhakikisha wananchi wa Mtwara wanaendelea kupata huduma ya majisafi na salama, wakati ukisubiriwa utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kutoa maji Mto Ruvuma, Serikali imeendelea kutekeleza kazi mbalimbali za kuboresha huduma ya maji kwa wananchi wa Mtwara Mjini ikiwemo uchimbaji wa visima vinne, ufungaji wa pampu tatu, ujenzi wa matanki matatu, ulazaji wa bomba kuu kilomita saba na bomba la usambazaji maji kilometa 27.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa vijijini, Serikali kupitia RUWASA inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 81. Miradi hii itakapokamilika itahudumia vijiji 285 ambapo jumla ya vituo vya kuchotea maji 1,562 vitajengwa/ kuboreshwa na inakadiriwa kunufaisha wananchi zaidi ya 454,375, hivyo, kuboresha utoaji wa huduma ya maji na kufikia wastani wa asilimia 79.91 kutoka asilimia 64 za sasa.