Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDD K. IDDI aliuliza:- Je, nili ni Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Geita – Bukoli hadi Kahama kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa niaba ya wananchi wa Msalala, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara hii imekuwa kero kubwa sana kwa wananchi, hususan wa Kata za Segese, Shilela, Ngaya na Bugarama. Barabara hii imeahidiwa kiasi cha dola milioni 40 kwa ajili ya kutengenezwa na Mgodo wa Barrick na imekuwa ni kero kubwa sana kwani inasababisha wakazi wa maeneo haya ambayo nimeyataja kuhama makazi yao asubuhi na kurudi jioni kutokana na vumbi kali kwa sababu inatumiwa na magari makubwa. Je, ni lini sasa Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Madini watakwenda kwa Waziri wa Fedha ili wamwambie Mheshimiwa Waziri wa Fedha aweze kutekeleza mkataba na makubaliano walioingia baina ya Serikali na Mgodi ili Mgodi uanze kutengeneza barabara hii mara moja? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni lini sasa Serikali itaanza kufikiria ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara inayotoka Kahama kupita Kata ya Busangi kwenda Nyang’hwale na kutokea Busisi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kassim Iddi Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Msalala kwamba katika jibu langu la msingi nimesema Mgodi wa Barrick wameonesha nia maana yake ni kwamba tayari timu ya majadiliano imeundwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Wizara ya Madini, lakini kwa sababu tunayojadili ni masuala ya fedha timu hiyo imejuimuisha pia Wizara yenyewe ya Fedha. Kwa hiyo, once majadiliano yatakapokuwa yamekamilika na kupata utaratibu sahihi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo itaanza kujengwa ili kuwapunguzia adha wananchi wake wa Lunguya, Segese, Ntobo hadi Bukoli na Geita ambao wako Mkoa wa Geita. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge aamini kwamba Serikali itafanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Nyang’hwale kwenda Busisi, naomba pia nimhakikishie kwamba ipo kwenye mipango, ipo kwenye Ilani na tuna mpango wa miaka mitano ambao nina hakika katika kipindi hiki barabara hiyo pia itajengwa kadiri fedha zitakavyopatikana. Ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. IDD K. IDDI aliuliza:- Je, nili ni Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Geita – Bukoli hadi Kahama kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli, alipopita kwenye Jimbo letu la Morogoro Kusini Mashariki alituahidi barabara ya Bigwa – Kisaki. Naomba kuiuliza Serikali barabara hii itaanza lini kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Babu Tale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alipotembelea Mkoa wa Morogoro, moja ya ahadi alizotoa na ilikuwa ni maagizo kwamba barabara hii ijengwe haraka kwa kiwango cha lami. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Babu Tale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki na wananchi anaowaongoza wa Jimbo lake kwamba barabara hii kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri itajengwa kwa kiwango cha lami kuanzia kilometa 50. Kama navyoongea naye mara kwa mara, nimhakikishie kwamba barabara hii itakuwa ni kati ya barabara ambazo zitatangazwa muda si mrefu kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)